Na Daniel Sichula – Mahakama, Mbeya
Jaji wa Mahama ya Rufani Tanzania Mhe. Ferdinand L.
Wambali hivi karibuni aliendeshea kikao cha awali cha kutathimini ya usikilizwaji
wa mashauri ya rufaa yaliyopangwa kuendeshwa na kikao cha Mahakama ya Rufani, Mahakama
Kuu Kanda ya Mbeya.
Aidha, Jopo hilo linaloundwa na Majaji Watatu wa
Mahakama ya Rufani chini ya Mwenyekiti wa kikao hicho Mhe. Wambali akiongozana
na Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Gerson J. Mdemu pamoja na Jaji wa
Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Latifa A. Mansoor
Akitoa taarifa ya kikao hicho cha tathmini Naibu
Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Omary H. Kingwele alielezea kuwa, taarifa
ya mashauri 26 ya rufaa yanayopaswa kusikilizwa ni pamoja na mashauri ya jinai
14 na mashauri ya madai 12
Wakati wa kikao hicho washiriki walipata wasaa wa
kuchangia maoni yao juu ya uendeshaji wa mashauri hayo na kutoa tathimini ya
namna uendeshaji wa mashauri hayo utakavyokua na namna wadua wote walivyojiandaa
katika kufanikisha mashauri yote 26 yanasikilizwa kwa muda muafaka uliowekwa.
Aidha, mwakilishi kutoka magereza aliahidi kuwafikisha
wafungwa wote mahakamani kwa wakati na wale wote walioko nje ya mkoa wa Mbeya
kuhakikisha kuwa wanafika kwa wakati pia.
Mhe. Wambali aliwasisitiza wadau wote kuhakikisha
nyaraka zote za rufaa zinapaswa kuwa tayari ili kurahisha usikilizwaji wa
mashauri yote yaliyopangwa kusikilizwa.
Akifafanua kasoro zinazojitokeza mara kwa mara ikiwemo
jambo linalohusu sababu za rufaa kufanana kwa kila mrufani Mhe. Mansoor alisema
“kwa mnao wasaidia warufani mjitahidi kuwaongoza vizuri wakata rufaa wenu,
sababu za rufaa siyo lazima ziwe nyingi unaweza kuandikia sababu za rufaa
chache na zenye mashiko.”
Mhe. Wambali aliwashukuru wadau wote walioshiriki
katika kikao hicho kwa maoni yao ya kuimarisha uendeshaji wa kikao kutoka
Taasisi mbalimbali mathalani Jeshi la Magereza, Maafisa wa Polisi, Mawakili wa
Serikali na Mawakili wa kujitegemea katika kuhakikisha na kufanikisha
usikilizwaji wa mashauri yote yaliyopangwa.
Vilevile, kikao hicho cha tathmini kilihudhuriwa Viongozi
wenyeji ambao ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga pamoja na Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe.
Aziza Emile Temu.
Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Ferdinand L. wambali akifungua kikao cha awali cha tathimini ya uendeshaji wa mashauri ya rufaa cha Jopo la Majaji wa Rufani kitakacho keti Mbeya, kulia ni Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mhe. Latifa A. Mansoor
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Mbeya
Mhe. Joachim Tiganga akitoa salaamu kwa jopo la Mahakama ya Rufani litakaloketi Mahakama Kuu Mbeya, kulia ni Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya
Mbeya Mhe. Aziza Emile Temu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni