Na Fredrick Mahava - Mahakama, Sumbawanga.
Naibu
Msajili wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Mhe. Joseph Luambano amewataka
watumishi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga kudumisha maadili, uadilifu na nidhamu ya hali
ya juu kazini.
Mhe.
Luambano amesema hayo leo tarehe 12 Juni, 2025 wakati wa kikao cha watumishi kilichofanyika katika
ukumbi uliopo Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga alipokuwa anawasilisha salamu za pongezi kwa
watumishi kutoka
Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Mahakama na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof.
Ibrahim Hamis Juma katika ziara iliyofanyika hivi karibuni katika Kanda hiyo.
“Baada ya kumaliza ziara, Tume inayo
furaha na fahari kubwa kutoa pongezi za
dhati kwa Mahakama Kuu ya
Tanzania Kanda ya Sumbawanga, kwa kazi nzuri na yenye kuleta tija katika
kutekeleza majukumu ya utoaji haki kwa wananchi. Hivyo naleta rasmi pongezi
hizo kwenu watumishi wa Mahakama kwa jinsi ambavyo mliweza kutoa ushirikiano
mkubwa kwa wajumbe wa Tume tokea mapokezi mpaka siku ya mwisho waliokuwa
wakiondoka katika Kanda yetu hongereni sana,” alisema Mhe. Luambano.
Naye, Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu
Essaba ambaye alikuwa Mwenyekiti wa kikao hicho alifungua kikao na kutaja agenga
za kikao hicho cha watumishi, pamoja na mambo mengine alisisitiza mshikamano
miongoni mwa watumishi na kufanya kazi kama timu moja
Vilevile, kikao hicho cha
watumishi kilishuhudia baadhi wa watumishi waliohudhuria Mafunzo, Semina na Makongamano
mbalimbali katika kipindi kilichopita walipata wasaa wa kuwasilisha taarifa zao.
Aidha, Afisa Hesabu Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Bw. Martin Mwandambo aliwasilisha
taarifa ya mgao wa fedha ya mwezi Mei, 2025.
Kikao hicho kilihudhuriwa
na watumishi kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga, Mahakama ya Hakimu Mkazi
Rukwa na Mahakama ya Wilaya Sumbawanga.
Naibu Msajili Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga akiwasilisha salamu za pongezi kutoka Tume ya Utumishi wa Mahakama.
Mtendaji
wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu Essaba (aliyesimama)
akifungua kikao cha watumishi.
Watumishi
wa Kada ya Ugavi wakiwasilisha taarifa yao baada ya kuhudhuria Kongamano la
wataalam wa Manunuzi na Ugavi
Watumishi
wa Mahakama Kada ya Sumbawanga Mwandishi Mwendesha Ofisi wakiwasilisha taarifa
yao baada ya kuhudhuria kongamano la Waandishi wwndesha ofisi (TAPSEA)
Watumishi
wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga wakisikiliza kwa makini wakati wa kikao hicho cha
watumishi.
Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni