Jumamosi, 14 Juni 2025

TANZIA; MTUMISHI WA MAHAKAMA KUU DIVISHENI YA KAZI AFARIKI DUNIA

Marehemu Michael Christian Kayombo enzi za uhai wake.


TANZIA

Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Mtumishi wake  Michael Christian Kayombo aliyekuwa akihudumu Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi kama Afisa Kumbukumbu Daraja la I.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na   Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi, Bw. Jumanne Muna, marehemu Kayombo alifikwa na umauti tarehe 13 Juni, 2025 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Bw. Muna amesema kuwa, taratibu za mazishi zinaendelea kufanyika, mazishi yanatarajiwa kufanyika Jumatatu tarehe 16 Juni, 2025 katika makaburi ya Kinyerezi-Tabata jijini Dar es Salaam. 

Marehemu Kayombo alizaliwa tarehe 10 Januari, 1992 na aliajiriwa Mahakama ya Tanzania tarehe 21 Septemba, 2015.

 Mahakama ya Tanzania inaungana na ndugu, jamaa na marafiki kuomboleza msiba huo wa kuondokewa na mpendwa wetu.

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, JINA LAKE LIHIMIDIWE. 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni