Ijumaa, 17 Oktoba 2025

JAJI MKUU AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA TUME YA USULUHISHI NA UAMUZI

Na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania leo tarehe 17 Oktoba, 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) kwenye ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma. 

Viongozi hao kutoka CMA wamepatiwa ushauri na maoni mbalimbali kutoka kwa Viongozi wa Mahakama yote yakilenga kuboresha huduma za utatuzi wa migogoro ya kazi zinazotolewa na Tume hiyo pamoja na kuboresha ushirikiano kati ya Tume na Mahakama.

Viongozi wa Mahakama walioshiriki katika mazungumzo hayo ni pamoja na Kaimu Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Abdi Kagomba, Kaimu Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Herbert, Makatibu Binafsi wa Jaji Mkuu, Mhe. Venance Mlingi na Mhe. Clarence Mhoja

Matukio katika picha mazungumzo kati ya Mahakama na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) leo tarehe 17 Oktoba, 2025 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (aliyeketi mbele) akiwa kwenye kikao na Viongozi kutoka Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) leo tarehe 17 Oktoba, 2025 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akizungumza jambo wakati wa kikao na Viongozi kutoka Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) leo tarehe 17 Oktoba, 2025 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya  Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.


Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Bw. Usekelege Mpulla (kushoto) akichangia jambo wakaati wa mazungumzo na Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (hayupo katika picha). Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi  Utawala wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Bi. Gift Kilimwomeshi.

Kaimu Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Abdi Kagomba (kulia) akichangia jambo wakati wa mazungumzo kati ya Mahakama na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) leo tarehe 17 Oktoba, 2025 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Kaimu Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Herbert (kushoto) 
akichangia jambo wakati wa mazungumzo kati ya Mahakama na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) leo tarehe 17 Oktoba, 2025 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma. Kulia ni Kaimu Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Abdi Kagomba.


Katibu Binasfi wa Jaji Mkuu ambaye pia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Mhe. Venance Mlingi akichangia jambo wakati wa mazungumzo kati ya Mahakama na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) leo tarehe 17 Oktoba, 2025 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Katibu Binasfi wa Jaji Mkuu, Mhe. Clarence Mhoja akiwa katika kikao kati ya Mahakama na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) leo tarehe 17 Oktoba, 2025 kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Viongozi kutoka CMA wakifuatilia mazungumzo wakati wa kikao na Viongozi wa Mahakama ya Tanzania wakiongozwa na Jaji Mkuu, Mhe. George Masaju.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Bw. Usekelege Mpulla (kushoto) akimkabidhi zawadi Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju leo tarehe 17 Oktoba, 2025 baada ya mazungumzo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Abdi Kagomba (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Bw. Usekelege Mpulla leo tarehe 17 Oktoba, 2025.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya Viongozi wa Mahakama na wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA).








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni