Mhe. Dkt. Angela Benedict Teye enzi za uhai wake.
TANZIA
Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha Mtumishi wake, aliyekuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Biashara.
Kwa mujibu wa Mtendaji wa Mahakama, Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara, Bw. Anatory Kagaruki Marehemu Dkt. Angela Teye alifikwa na umauti tarehe 16 Oktoba, 2025 katika Hospitali ya John Muir 'Medical Center' iliyopo Walnut Creek mjini California nchini Marekani alipokuwa akipatiwa matibabu.
Bw. Kagaruki amesema taratibu na mipango ya mazishi inaendelea kuratibiwa na familia.
Marehemu Dkt. Teye aliajiriwa na Mahakama ya Tanzania kwa Cheo cha Hakimu Mkazi tarehe 29 Juni, 2007 na kupangiwa Kituo cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Tanga.
Mahakama ya Tanzania inaungana na ndugu, jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha kuomboleza msiba huo mzito wa kuondokewa na Mpendwa wetu.
BWANA
ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni