Na Mwandishi Wetu
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina,
tarehe 10 Oktoba 2025, amekabidhi Juzuu za Maamuzi ya Migogoro ya Kazi kwa Chuo
cha Ustawi wa Jamii.
Mhe.
Dkt. Mlyambina alikabidhi nakala mbili (2) za Juzuu za Maamuzi ya Migogoro ya
Kazi Mahakama Kuu ya Tanzania pamoja na nakala sabini (70) za Labour Court Case
Digest, akiwa ameambatana na mahakimu wa Mahakama Kuu.
Akizungumza
katika makabidhiano hayo, Jaji Dkt. Mlyambina amesema kuwa kuleta Juzuu hizo
Chuo cha Ustawi wa Jamii ni heshima ya kutambua mchango na kazi inayofanywa na
Chuo cha Ustawi wa Jamii, ambacho ni Chuo pekee nchini kinachotoa taaluma za
kazi na kuzalisha maafisa wanaokwenda kufanya kazi katika Mahakama za kazi kama
wasuluhishi na watatuzi wa migogoro ya ajira.
Aidha,
Juzuu hizo zimepokelewa na Naibu Mkuu wa Chuo - Fedha na Utawala, Dkt. Eventus
Mugyabuso, kwa niaba ya Mkuu wa Chuo hicho.
Kadhalika
Juzuu za Maamuzi ya Migogoro ya Kazi zinahusu kesi zilizotolewa maamuzi kuanzia
mwaka 2010 hadi 2024, na zinatarajiwa kusaidia wanafunzi, wanazuoni wa sheria
na watafiti kupata rejea sahihi na kuelewa mwenendo wa tafsiri za kisheria katika
migogoro ya ajira nchini.
Kwa Upande wake Naibu Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Dkt. Eventus Mugyabuso amemshukuru Jaji Mlyambina kwa kuona umuhimu wa kuleta Juzuu hizo chuoni hapo ambazo zitaongeza ujuzi kwa wanafunzi wa Taaluma za kazi na wanazuoni kwa ujumla.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Kazi, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina (wa tatu kushoto) akikabidhi Juzuu za Maamuzi ya Migogoro ya Kazi kwa Chuo cha Ustawi wa Jamii.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni