Na. Rehema Awet – Mahakama, Mwanza
Mwili wa marehemu Fredrick Binamungu Kakurwa aliyekuwa
Hakimu Mkazi II Mahakama ya Mwanzo Nyanchenche umeagwa tarehe 13 Oktoba, 2025 nyumbani
kwake maeneo ya Kabwalo Buswelu Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.
Ibada ya kuaga mwili wa marehemu ilihudhuriwa na
Majaji wa Mahakama ya Rufani wakiongozwa na Mhe. Winifrida Beatrice Korosso,
Majaji wa Mahakama Kuu, Mahakimu wa Mkoa wa Mwanza pamoja na viongozi
mbalimbali wa Mahakama Kanda ya Mwanza.
Mtendaji wa Mahakama Kanda ya Mwanza, Bw. Tutubi
Deo Mangazeni alitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Mahakama na kuwapa pole wafiwa
wote wakiwemo familia, ndugu jamaa marafiki na wafanyakazi wenzake waliohudhuria
ibada ya kuaga mwili wa marehemu.
Aidha, kwa masikitiko makubwa alieleza namna
ambavyo Mahakama imepata pengo kwa kuondokewa na mfanyakazi wake ambaye alikuwa
kijana hodari na mchapakazi.
Vilevile, alieleza kuwa Mahakama kama mwajiri
ilivyoshiriki katika taratibu zote za kuhifadhi na hatimaye kuusafirisha mwili
wa marehemu kwa ajili ya kuupumzisha kwenye nyumba yake ya milele huko kijijini
kwao ambapo mazishi yamepangwa kufanyika mnamo tarehe 14 Octoba, 2025
Baada ya ibada ya kuaga mwili wa marehemu,
ulisafirishwa kuelekea kijijini kwao Bundaza Kata ya Nyakibimbili mkoani
Kagera.
Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya
Mwanza, Bw.Tutubi Deo Mangazeni akiaga mwili wa marehemu Fredrick Binamungu
Kakurwa.
Sehemu ya Majaji, Wasajili na Mahakimu wa Mahakama ya Tanzania wakishiriki
Ibada ya kuuaga mwili wa marehemu Fredrick Binamungu Kakurwa, kushoto ni Jaji
wa Mahakama ya Rufani Mhe. Winifrida Beatrice Korosso akiwaongoza Majaji
wenzake Mhe. Penterine Kente na Mhe. Amour Khamis, wengine ni Majaji wa Mahakama
Kuu Kanda ya Mwanza Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Mhe. Dkt. Ntemi
Kilekamajenga, Mhe. Kassim Robert, Mhe. Emmanuel Ngigwana na Mhe. Kamana
Kamana, Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Mhe. Janeth Musaroche na Hakimu
Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Mwanza Mhe. Erick Marley
Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe.
Winifrida Beatrice Korosso akiaga mwili wa marehemu Fredrick Binamungu Kakurwa
Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya
Mwanza, Mhe. Kamana S Kamana akiaga mwili wa marehemu Fredrick Binamungu
Kakurwa.
Sehemu ya waombolezaji na watumishi wa Mahakama
Kanda ya Mwanza wakishiriki kuaga mwili wa marehemu Fredrick Binamungu Kakurwa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni