Jumatatu, 13 Oktoba 2025

TANZIA; MTUMISHI WA MAHAKAMA AFARIKI DUNIA

 TANZIA


Marehemu Fredrick Binamungu Kakurwa enzi za uhai wake.

Mahakama ya Tanzania inasikitika kutangaza kifo cha mtumishi wake wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mwanza Mhe. Fredrick Binamungu Kakurwa aliyekuwa ameajiriwa kwa nafasi ya Hakimu Mkazi II akihudumu Mahakama ya Mwanzo Nyancheche iliyopo wilaya ya Sengerema.

Kifo hicho kilitokea mnamo tarehe 10 Oktoba, 2025 majira ya saa nne usiku eneo la Kiseke wilaya ya Ilemela akielekea nyumbani, akitokea kazini kwake Mahakama ya Mwanzo Nyancheche iliyopo wilaya ya Sengerema

Kwa mujibu wa Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Bw. Tutubi Mangazeni, marehemu Bw Fredrick Binamungu Kakurwa alifikwa na umauti kutokana na ajali ya pikipiki iliyotokea eneo la kiseke.

Marehemu Fredrick aliajiriwa mnamo tarehe 28 Novemba, 2024 kama Hakimu Mkazi II na kupangiwa kituo cha kazi Mahakama ya mwanzo Nyancheche ambako amehudumu mpaka umauti ulipomfika.

Wakati wa ajira yake marehemu alikuwa na elimu ya shahada ya sheria na Astashahada ya mafunzo ya sheria kwa vitendo kutoka Chuo cha Sheria Tanzania (Law school of Tanzania).

Marehemu Fredrick anatarajiwa kuzikwa mnamo tarehe 14 Octoba, 2025 nyumbani kwao, kijiji cha Bundaza, kata ya Nyakibimbili mkoani Kagera.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni