- Wajipanga kushughulikia na kudhibiti mashauri ya mlundikano
Na AIDAN
ROBERT, Mahakama-Kigoma
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba
Rwizile ametoa rai kwa viongozi wa Mahakama za Wilaya zilizopo ndani ya Kanda
hiyo kuongeza mikakati pamoja na ushirikiano katika uamuzi wa mashauri na
kuzuia mashauri ya mlundikano sambamba na kuwa na usimamizi mzuri wa rasilimali
fedha zinazoletwa kwa ajili ya
kuendeshea shughuli za Mahakama.
Mhe.
Rwizile alitoa rai hiyo tarehe 25 Oktoba 2025 katika ukumbi wa mikutano
Mahakama Kuu Kigoma kwenye kikao cha Kamati ya Uongozi cha Tathmini
ya shughuli za Mahakama kwa robo ya pili ya mwaka kilicholenga kuweka mikakati wa
kutekeleza Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania wa mwaka 2025/2026 hususani
nguzo ya pili ya Upatikanaji na Utoaji Haki kwa wakati.
Jaji
Mfawidhi huyo vilevile, alitoa pongezi kwa juhudi za kila mtumishi katika eneo
lake kwa kuwa na ushirikiano akieleza kuwa, ushirikiano ndio unaleta matokea
mazuri ya utendaji. Aidha, pongezi zingine alizitoa kwa Mahakama za Wilaya
Buhigwe na Uvinza kwa uhifadhi wa mazingira kwa kupanda miti ya matunda na mbao
na kuleta mandhari nzuri na hewa safi.
Aidha, aliongeza kusema, “tuongeze weledi wa kusikiliza mashauri kwa njia ya mtandao (virtual Court) ili kuhakikisha mashauri ya Ardhi, Benki na yale ya biashara yanasikilizwa na kumalizika mapema ipasavyo ikiwa ni sambamba na fedha za mirathi zilizopo katika akaunti ya mirathi zinalipwa kwa wanufaika kwa wakati.”
Pamoja na hayo, Mhe. Rwizile aliwaongoza Viongozi hao katika zoezi la upandaji miti Mahakama ya Wilaya Kigoma na kufanya mazoezi ya viungo ikiwa ni utamaduni wa Mahakama Kanda Kigoma ili kuimarisha afya za watumishi katika utendaji wa kila siku wa shughuli za Mahakama.
Kwa upande
wake Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma, Bw. Filbert Matotay alisema, umeandaliwa
mpango maalum wa kusikiliza mashauri yanayokaribia kuingia katika mlundikano na
kuendelea kusimamia vizuri rasilimali zilizopo ili zilete tija na kuhakikisha
inafikiwa ili kuendeleza mpango wa kuongeza vifaa vya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano (TEHAMA) hususani Kompyuta Mpakato.
Bw. Matotay alisema lengo la Kanda hiyo ni kuendeleza
ushirikiano na wadau na kuimarisha maslahi ya watumishi na maadili ya kazi
katika kuendeleza programu ya kupanda miti ya mbao na matunda katika maeneo ya
majengo yote ya Mahakama Kanda ya Kigoma na kukamilisha programu ya Mahakama
bila matumizi ya karatasi (Paperless Court).
Naye Naibu
Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Fadhili Mbelwa
alisema kuwa, Mahakimu Wakazi Wafawidhi waainishe maeneo ambayo watumishi na
wadau wa Mahakama wanaweza kupewa mafunzo ya ndani katika kuboresha shughuli za
Mahakama pamoja na Kwenda na na kasi ya
usikilizwaji wa mashauri mapema ipasavyo na kwa njia ya Mahakama Mtandao.
Hata hivyo,
Mhe. Mbelwa aliwakumbusha Wafawidhi hao kuongeza usimamizi katika eneo la
mashauri ili kuzuia mlundikano wa mashauri katika vituo vyao.
Wajumbe waliohudhuria kikao hicho walikuwa Mahakimu Wakazi Wafawidhi wa Mahakama za Wilaya mkoani Kigoma, Wakuu wa Idara za Mahakama Kuu Kigoma na Maafisa Tawala kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma, Mahakama za Wilaya Kigoma, Kibondo, Uvinza, Kasulu, Buhigwe na Kakonko.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba
Rwizile akisisitiza jambo hivi karibuni wakati wa Kikao cha Kamati ya Uongozi wa Mahakama
Kanda ya Kigoma kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Kigoma.
Wajumbe wa kikao wakifuatilia kwa makini taarifa ya utendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma wakati wa Kikao cha Kamati ya Uongozi wa Mahakama Kanda ya Kigoma kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Kigoma.
Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya
Kigoma, Bw. Filbert Matotay akifafanua jambo kwa msisitizo wakati wa kikao cha Kamati ya Uongozi wa Mahakama Kanda ya Kigoma kilichofanyika
katika ukumbi wa mikutano uliopo kwenye jengo la Mahakama hiyo.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba
Rwizile akipanda mti wa mchikichi katika eneo la wazi lililopo Mahakama ya
Wilaya Kigoma mara baada ya kumaliza
Jaji wa
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. John Francis Nkwabi akipanda
mti wa mchikichi katika eneo la wazi lililopo Mahakama ya Wilaya Kigoma mara
baada ya kumaliza kikao
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya
Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa kikao
(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni