Na. Innocent Kansha – Mahakama, Ngorongoro
Watumishi
wa Mahakama Kuu Masjala Kuu Dodoma wamefanya ziara ya kutembelea Mbuga ya
Hifadhi ya Ngorongoro kujionea vivutio mbalimbali vya mbuga hiyo ikiwa ni
mkakati wa kutanganza utalii wa nadani na kujifunza utunzaji wa mazingira na
ekolojia ya mazingira, zira hiyo ya kitalii ilifanyika tarehe 17 na 18 Oktoba,
2025 katika bode hilo maarufu Dunia lenye wanyama Pori mbalimbali ikiwemo wale
wanyama watano maarufu Duniani.
Akizungumza
kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati wa maandalizi wa ziara hiyo wakati wa
kuhitimisha ziara mratibu wa ziara hiyo Afisa Utumishi kutoka Mahakama Kuu Masjala
Kuu Dodoma Bi. Edith Kajuna amesema lengo la ziara hiyo ni kuitangaza Tanzania kwa
Dunia kwamba kuna vivutio vizuri sana vya mbuga za wanyama na vivutio vingine
kama Mlima Kilimanjaro ambao upo miongoni mwa maajabu saba ya Dunia.
“Si
lazima tuwategemee wageni kutoka nje ndiyo waje kuvitangaza vivutio vyetu ni
sisi wenye kuweza kuona kwamba tunamaeneo, tunavivutio vya kila aina na tuna
maeneo ya utalii ambao tunaweza kuvitangaza sisi na kuufanya wenyewe hivyo
kuvutia watu wengi kwa maana watalii wa ndani,” alisema Bi. Kajuna.
Akifafanua
malengo ya ziara hiyo ya utalii wa ndani alisema ilikuwa kutoa elimu kwa jamii
hasa kuhusu masuala ya kisheria na kuutangazia umma kwamba sasa Makao Makuu ya
Mahakama yapo Dodoma, kwa kutoa machapisho mbalimbali ya kimahakama yanayo
onesha kuwa sasa mahitaji yote ya kisheria yanapatikana Makao Makuu ya Mahakama
Dodoma.
“Watumishi
wote kama wanavyofahamu mdhamina wa ziara hii ya utalii katika bonde la
Ngorongoro ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed
Siyani na Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Kuu Bw. Leonard Magacha waliowezesha
kwa namna moja au nyingine kufanikisha safari hii hivyo timu zima ya watumishi
inatoa kongole za dhati,” aliongeza Bi Kajuna.
Aidha,
Bi. Kajuna ameongeza kuwa, kupitia ziara hiyo wamejifunza mambo mengi sana
walitarajia kuwaona wanyama watano wale maarufu Dunia lakini kupitia ziara hiyo
walifanikiwa kuwaona wanyama nne ambao ni Simba, Faru, Twiga na Tembo na wengine
wakiwemo kiboko, nyati, nyumbu, pundamilia, sungura, swala, kasongo, fisi, na ndege mbalimbali kama bata, mbuni, cowbird
na uoto wa asili wa kuvutia sana. Vitu hivyo vyote vinavutia sana kuweza
kumvutia kila mtalii kuweza kuja kujionea vitu gana ambavyo vinapatikana ndani
ya hifadhi ya Ngorongoro.
“Tunatoa
rai kwa Taasisi, Idara, Mashirika na watumishi wa umma na binafsi kuweza
kujionea mambo mbalimbali ambayo yanapatikana kwenye Mamlaka ya hifadhi ya
Ngorongoro,” amesisitiza Bi. Kajuna.
Akitoa
wito kwa wananchi Bi. Kajuna amesema wananchi wanapaswa kujitoa na kupenda nchi
yao na kupenda kufanya utalii lakini pia kuitangaza Tanzania nje ya mipaka
yake. Aidha alihimiza utunzaji wa mazingira kwasababu utunzaji wa mazingira
unasaidia uoto wa asili kuendelea kuwepo na historia ya wanayama pamoja na
mimea mingine yote kuendelea kuwepo.
“Tunapoharibu
mazingira tunafanya uoto wote wa asili unapotea wanyama wote wanatoweka, kwa
hiyo tuendelee kupambana kwa ajili ya kuiweka Tanzania iendelee kuwa ya kijana,
iendelee kuvutia na kila mtu anayeingia kwenye hifadhi zetu aweze kutamani
kurudi tena,” amesema Bi. Kajuna.
Kwa
upande wake mratibu wa ziara hiyo ambaye ni Afisa Usafrishaji kutoka Mahakama
Kuu ya Tanzania Masjala Kuu Dodoma Bw. Richard Dotto William amesema kuwa,
ziara ilikuwa na malengo mbalimbali ikiwemo kujifunza masuala ya utalii na
kuunga juhudi za kukuza utalii wa ndani.
Vilevile
ziara ililenga kuboresha afya ya akili na kupumzisha akili hasa kutokana na
majukumu ya kila siku ya kiutumishi na kujifunza namna Taasisi zingine
zinazofanya kazi na Mahakama ya Tanzania zinafanya kazi kwa ufanisi katika majukumu
yao ya kulijenga taifa la Tanzania.
Akatoa
rai kwa Taasisi nyingine ziweze kuona umuhimu wa kufanya utalii hasa utalii wa
ndani pamoja na kutunza mazingira ili kufanya utalii uwe endelevu na kudumisha
hifadhi pamoja na misitu ya Tanzania kwa ujumla.
“Nawashauri
viongozi na Taasisi zingine ziwe na utaratibu huu walau wa mara moja kwa mwaka
katika kuwapa watumishi wao ama kutoa nafasi kwa watumishi ambao watakuwa
tayari kwa ajili ya kutemebelea vivutio na maeneo mbalimbali ya kitalii ili
kujifunza, kufanya mambo yanayohusiana na utalii na utunzaji wa mazingira ili nchi
ya Tanzania iimarike katika sekta ya utalii,” amesema Bw. William.
Naye
Mwakilishi kutoka Kampuni ya Utalii ya Dodoma Safari Tour Bw. Billali Ally
amesema, anamshukuru Mungu kwa kupata nafasi ya kutembelea hifadhi ya Bonde la
Ngorongoro na kujifunza mambo mbalimbali kama inavyosomeka kwenye vitabu
Ngorongoro ni sehemu yenye umashuhuri mkubwa sana Duniani.
“Lengo
letu kubwa ilikuwa kuja kupata uzoefu wa maisha mengine ya wanyama jinsi
wanavyoishi na kujifunza vitu mbalimbali vya ekolojia ya maisha ya wanyama na
kufurahisha akili zetu kwa mwaka mzima tunakuwa na shughuli mbalimbali za
kufanya kazi na vitu vingine, kunawakati inabidi tupumzishe akili ni miongoni
mwa malengo yaliyosababisha tuje kutembelea hapa hifadhi ya Ngorongoro,”
amesema Ally.
Aidha, ameongeza kuwa kusafiri na watumishi wa Muhimili wa Mahakama ni jambo moja lililowapa uzoefu mkubwa kampuni ya Dodoma Safari Tour ya kuunganisha umoja na Taasisi ya Mahakama katika kutekeleza majukumu yao ya kuendesha shughuli za kiutalii kwa kutambulisha hifadhi za Taifa na kuunganisha wadau wengi wa utalii ili kukuza utalii wa ndani nchini Tanzania.
Moja ya Big Five akiwa amepumzika mara baada ya hekaheka zake za mawindo katika Mbuga ya Hifadhi ya Ngorongoro





















Hakuna maoni:
Chapisha Maoni