Alhamisi, 5 Februari 2026

MAHAKAMA DODOMA, WADAU WAKUTANA KUTATHMINI UTENDAJI

Na ARAPHA RUSHEKE, Mahakama – Dodoma.

Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, hivi karibuni ilifanya kikao na wadau ili kutathmini utendaji kazi wa mwaka 2025 na kuweka mikakati ya kuboresha huduma za utoaji haki kwa mwaka 2026.

Kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Dodoma, kilifunguliwa na Jaji Mfawidhi, Mhe. Dkt. Juliana Masabo. Mhe. Dkt. Masabo alieleza kuwa kikao hicho ni sehemu ya utamaduni wa Mahakama kukutana na wadau wake ili kufanya tathmini ya pamoja na kubadilishana uzoefu wa namna bora ya kuboresha utoaji wa huduma.

Mhe. Dkt. Masabo alieleza kuwa lengo lingine ni kuangalia kwa pamoja utendaji kazi wa mwaka uliopita, kubaini mafanikio na changamoto zilizojitokeza, na kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha maeneo yaliyohitaji uboreshaji.

Alisisitiza kuwa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, inayojumuisha Mikoa ya Dodoma na Singida, ina wajibu mkubwa kutokana na Dodoma kuwa Makao Makuu yaNnchi, hivyo mabadiliko yanayoendelea yanahitaji kasi na ubora zaidi katika utoaji haki.

Aidha, alibainisha lengo jingine ni kuimarisha ushirikiano kati ya Mahakama na wadau, ambao ni nguzo muhimu katika utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Mahakama. Kupitia vikao vya namna hiyo, wadau wamekuwa wakipanga pamoja na kutekeleza majukumu kwa pamoja, jambo lililochangia kuongeza ufanisi wa utendaji.

Akizungumzia mafanikio ya mwaka uliopita wa 2025, Mhe. Dkt. Masabo alisema Mahakama ilipokea mashauri zaidi ya 1,000 na pia kufanikiwa kumaliza mashauri zaidi ya 1,000. Alibainisha kuwa mafanikio hayo yametokana kwa kiasi kikubwa na ushirikiano wa wadau mbalimbali, wakiwemo Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mawakili wa Kujitegemea, Mabaraza ya Ardhi, Ofisi ya Kamishna wa Ardhi, Msajili wa Hati, pamoja na Taasisi nyingine zinazohusika na masuala ya kisheria na kiutawala.

Aliongeza kuwa mashauri mengi yaliyopokelewa na kumalizwa yalihusu masuala ya ardhi, jambo linaloonesha umuhimu wa ushirikiano wa karibu na taasisi zinazohusika na sekta hiyo.

Katika kikao hicho, wadau walipata pia fursa ya kujifunza mambo mbalimbali zitakazowasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Akisoma taarifa ya mashauri katika kikao hicho, Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mhe Silivia Lushasi, alibainisha mikakati mbalimbali ya kuzuia mashauri kukaa muda mrefu mahakamani kwa mwaka 2026.

Meza kuu ikiongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo [aliyepo katikati] ikiwa inasikiliza kwa makini maoni na ushauri kutoka kwa wadau waliodhuria kikao hicho, aliyepo kulia kwake ni Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mhe. Amir Mruma na aliyepo kushoto kwake ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mhe. Silvia Lushasi.

Washiriki wa kikao wakiogozwa na Jaji Mfawdhi (hayupo pichani) wakisikiliza kwa makini wasilisho kutoka kwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Silivia Lushasi (hayupo pichani).

Meza kuu ikiongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo [aliyepo katikati] ikiwa katika picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama Kuu Dodoma pamoja Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali waliohudhuria kikao hicho, walioketi kulia kwake ni Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mhe. Amir Mruma na aliyepo kushoto kwake ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mhe. Silvia Lushasi.

Meza kuu ikiongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo [aliyepo katikati] ikiwa katika picha ya pamoja na Mahakimu pamoja na wadau kutoka Taasisi mbalimbali waliohudhuria kikao hicho.

Meza kuu ikiongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo [aliyepo katikati] ikiwa katika picha ya pamoja na Si.ekretariet  

 Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Morogoro.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni