Na FRANCISCA SWAI-Mahakama, Musoma
Watumishi wa Mahakama Kuu
ya Tanzania, Kanda ya Musoma, jana tarehe 04 Februari 2026, walitembelea Kituo
cha Watoto wenye mahitaji maalum na kutoa msaada wa vitu mbalimbali muhimu.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu ya Tanzania, Kanda ya Musoma, Mhe. Fahamu Mtulya, aliwaongoza watumishi hao,
ambao walitembelea Kituo cha Al-Jaziira Orphan Centre kilichopo Kijiji cha
Mkirira, Kata ya Nyegina, Musoma Vijiji. Kituo hicho kinahudumia watoto wa
kiume wenye umri wa miaka minne hadi 15.
Akitoa shukrani kwa
watumishi wa Mahakama, Kaimu Meneja wa Kituo hicho, Bw. Said Masaka, alisema Kituo
hicho kina mahitaji mengi, ikiwa ni pamoja na elimu ya ushauri wa kisheria
kuhusu haki za motto, mafunzo ya sheria ya mtoto kwa walezi na watumishi, pamoja
na msaada wa kusimamia sera ya ulinzi wa mtoto.
Ombi hilo lilipokelewa na
uongozi wa Mahakama ambapo waliahidi kwenda kujipanga ili kuwapa elimu hiyo
hivi karibuni.
Aidha, pamoja na tendo jema hilo, watumishi wa Mahakama walipata pia elimu kuhusiana na masuala ya kibenki na fedha kutoka kwa watumishi wa Benki ya NMB Musoma.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni