Na FRANCISCA SWAI-Mahakama, Musoma
Jopo la Majaji watatu wa
Mahakama ya Rufani wapo mjini Musoma kwa ajili ya usikilizaji wa mashauri 48
kwenye kikao kitakachofanyika kwenye masjala ndogo iliyopo katika jengo la
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Musoma.
Kikao hicho kilichoanza
tarehe 09 Februari, 2026 kitahitimishwa tarehe 06 Machi, 2026. Kinaongozwa na Mhe. Dkt. Gerald Ndika ambeye
ni Mwenyekiti. Majaji wengine wanaounda jopo hilo ni Mhe. Patricia Fikirini na
Mhe. Mustapha Ismail.
Usikilizaji wa mashauri
hayo ulitanguliwa na kikao cha maandalizi (Pre Session), huku Majaji wakisisitiza
Wadau kukamilisha maandalizi yao mapema, kuzingatia muda ili kuhakikisha mashauri
yanasikilizwa kama ilivyopangwa.
Kwenye kikao hicho, kwa
mujibu wa Naibu Msajili, Mhe. Omary Kingwele, mashauri yatakayosililizwa ni rufaa
mbili za madai na mengine yanahusu jinai.
Kabla ya kuanza kikao
hicho, Jopo la Majaji hao lilipata nafasi ya kusalimiana na watumishi wa
Mahakama Kuu Musoma pamoja na Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma. Watumishi hao
waliwakaribisha Majaji hao na kuahidi kuwapa ushirikiano.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Mbeya.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni