Jumatano, 18 Februari 2026

TANZIA: HAKIMU MAHAKAMA YA MWANZO MIKESE AFARIKI DUNIA


Mhe. Asajile Joshua Mhando enzi za uhai wake.

Kaimu Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro, Mhe. Stephen M. Magoiga, anasikitika kutangaza kifo cha Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Mwanzo Mikese, Mhe. Asajile Joshua Mhando, aliyefariki Dunia tarehe 17 Februari, 2026 saa 7.00 mchana katika Hospitali ya Platnum mjini Morogoro alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kujisikia vibaya akiwa kazini.

Taratibu za mazishi zinaendelea kuratibiwa, na mara baada ya kukamilika zitatolewa.

Uongozi wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro unatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na watumishi wote kwa msiba huu mzito.

Bwana alitoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni