- Awashukuru watumishi wote Kigoma
- Awasisitiza kufanya kazi kwa maadili bila kuacha nyuma mazoezi kwa afya
Na AIDAN ROBERT,
Mahakama-Kigoma
Jaji wa
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma, Mhe. Projestus Kahyoza tarehe 24 Machi,
2026 aliwaaga watumishi wa Kanda hiyo mara baada ya kupata uhamisho wa Kituo
cha kazi kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma kuelekea Kanda ya Tabora.
“Nimepokea
barua ya uhamisho wa kituo cha kazi ikinihamisha kutoka Kigoma kuelekea
Mahakama Kuu Kanda ya Tabora, hivyo naomba kuwaaga na kutoa shukrani kwa Jaji
Mfawidhi, Mhe. Augustine Rwizile na Mhe. John Nkwabi na watumishi wote kwa
ushirikiano wenu wa dhati katika kipindi chote nilichohudumu katika Kituo hiki
cha Kigoma,” alisema Jaji Kahyoza.
Vilevile,
alitoa rai kwa watumishi wote wa Mahakama Kanda ya Kigoma kutoaacha kufanya mazoezi
ya viungo kwani ndio mtaji na msingi wa ufanisi na tija katika shughuli za
mfanyakazi kwa mwajiri wake.
Aidha,
alisema kuwa, ataendelea kuwa mdau wa mazoezi na huko aendako kwani afya ndio
jambo muhimu la kwanza kwa mwanadamu, hivyo ameisisitiza Klabu ya Mazoezi Kigoma
iendelee kwakuwa ndio msingi wa utendaji kazi wenye tija kwa mwajiri.
kwa upande
wake Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Rwizile
akizungumza kwa niaba ya watumishi wa Kanda ya Kigoma, alimshukuru na kumtakia
kila la heri Jaji Kahyoza katika kituo chake kipya.
Alimshukuru
pia kwa ushirikiano wake kwa kipindi chote alipokuwa akihuduma katika kituo cha
Kigoma na hivyo kumtaka kuendelea na juhudi zake za kupiga kazi kama
alivyofanya Mahakama Kanda ya Kigoma.
“Kuondoka
kwa Mhe. Kahyoza kunapunguza nguvu katika usikilizwaji wa mashauri katika Kanda
yetu, hata hivyo Kanda tumejipanga kuhakikisha mashauri yanayosajiliwa
yanasikilizwa na kuamriwa kwa haraka ili kuendana na Dira ya Mahakama ya Utoaji
wa Haki sawa kwa wote mapema ipasavyo,” alisema Jaji Rwizile.
Jaji Projestus Kahyoza akizungumza na watumishi wa Mahakama Kanda ya Kigoma juu ya uhamisho wake na kutoka Kanda hiyo na kuhamishiwa Makahama Kanda ya Tabora.
Watumishi
wa Mahakama Kanda ya Kigoma wakipokea taarifa ya uhamisho wa aliyekuwa Jaji wa Mahakama
Kuu Kanda ya Kigoma, Mhe. Projestus Kahyoza ambaye amehamishiwa Mahakama Kuu Kanda ya Tabora.
Jaji Kahyoza (wa kwanza kulia) akiwaaga wanamazoezi katika eneo la kufanyia mazoezi lililopo juu ya jengo la Mahakama hiyo.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma, Mhe. Augustine Karichuba Rwizile (kulia) na Afisa Utumishi wa Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma, Bw.
Festo Sanga wakipiga zoezi la (push up) wakati wakimuaga mwanamazoezi mwenzao, Mhe. Kahyoza. Waliosimama ni watumishi wanamazoezi wa Kanda hiyo wakati wa kuwaaga
wanamazoezi wenzao Mhe. Projestus Kahyoza,
na aliyekuwa Mtendaji wa Mahakama, Bw. Filbert Matotay (aliyevaa fulana la kahawia) ambaye naye amehamishiwa Mahakama Kuu Kanda ya Singida.
Picha ya
wanamazoezi wakifurahia kinywaji maalum kwa ajili ya kuwaaga wanamazoezi
wenzao wanaohamishwa Kituo cha kazi ambao ni
Jaji, Mhe. Projestus Kahyoza na Bw. Filbert
Matotay, Mtendaji wa Mahakama.
(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni