Na. Fredrick Mahava- Mahakama, Sumbawanga
Watumishi
Wanawake wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga wameshiriki katika Maadhimisho ya
siku ya Wanawake Duniani kwa kushiriki katika shughuli mbalimbali kama vile kufanya
matendo ya huruma na kushiriki mafunzo ya ujasiriamali.
Maadhimisho hayo ya mwaka 2026 yanafanyika na
kuadhimishwa kuanzia ngazi ya Kata. Kwa upande wa Kata ya Katandala maadhimsho
hayo yamefanyika tarehe 2 Machi 2026 yakiongozwa na Diwani wa Kata hiyo Mhe.
Edwin Misasi.
Maadhimisho
hayo yalianza kwa Maandamano yaliyoanzia Ofisi ya Kata ya Katandala kuelekea
katika kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi cha
Bethania ambapo mahitaji mbalimbali ya watoto yalitolewa.
Kwa
upande wake Mhe. Deontinta Kashaija ambaye alikuwa Mkuu wa Msafara wa Watumishi
wanawake wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga wakati anakabidhi mahitaji kwa watoto
alisema, walichanga pesa ili kufanikisha upatikanaji wa mahitaji hayo na pia
waliwashirikisha baadhi ya wanaume ambao waliguswa na kuchangia na hivyo kuweza
kupatikana kwa mahitaji hayo.
Naye,
Mkurugenzi wa Kituo cha Bethania aliwashukuru wanawake wote kwa kuwaletea
watoto hao mahitaji muhimu ambayo yatawasaidia. Vilevile aliwaomba wawe
wanakuja kuwatembelea watoto hao mara kwa mara kwani watoto hao wanafarijika
wanapotembelewa na watu mbalimbali.
Aidha,
alieleza kuwa wana Vituo viwili vya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu
yaani kile cha watoto wadogo wa chini ya miaka 10 na kile cha watoto kuanzia
miaka 10 na kuendelea.
Baada
kumaliza kutoa mahitaji kwa watoto wa kituo cha Bethania maandamano hayo yalielekea
katika Ofisi ya Tarafa ya Lwiche ili kuendana na kauli mbiu ya mwaka isemayo “Haki kwa wanawake na wasichana: msingi wa
Maendeleo Jumuishi kufikia Dira 2050” Wanawake walikusanyika katika ukumbi
uliopo ofisi ya taarafa ya Lwiche na kupewa mafunzo mbalimabali kuhusu ujasiliamali, elimu kuhusu malezi
na makuzi ya watoto na elimu kuhusu fursa mbalimbali zilizopo katika maeneo
jamii.
Vilevile
Taasisi za kifedha kama NMB walipata fursa ya kutoa elimu kwa wanawake kuhusu
mikopo ya masharti nafuu inayotolewa kwa vikundi mbalimbali na namna gani
wanawake wanaweza kunufaika na fursa hizo. Pia walipata wasaa wa kujua fursa ya
mikopo inayotolewa na Serikali na kusimamiwa na benki ya NMB ambayo kipaumbele chake
wanapewa wanawake.
Nao
Jeshi ya Zimatoto na Uokoaji walitumia jukwaa hilo kutoa elimu kwa wanawake
kuhusu mambo mbalimbali yanayohusu namna ya kupambana na majanga ya moto
kuanzia ngazi ya familia na kuelezea huduma muhimu zinazotolewa na Jeshi hilo ikiwa ni pamoja namna ya kutoa taarifa kwa
Jeshi hilo pindi unapopata majanga ya Moto.
Aidha,
wakati wa Mafunzo hayo wanawake walipata wasaa wa kuuliza maswali mbalimbali
kwa kila mada iliyofundishwa na wawezeshaji walitoa ufafanuzi ili kuongeza
uelewa kwa washiriki wa mafunzo hayo. Baada
ya mafunzo wanawake walihimizwa kushiriki kilele cha siku ya wanawake
duniani itayofanyika tarehe 08 Machi 2026.
Picha
ya watumishi wanawake wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga wakati wa maadhimisho ya
siku ya wanawake katika Kata ya Katandala Sumbawanga Mjini.
Afisa
kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji akitoa elimu kuhusu namna ya kupambana na
majanga ya moto wakati wa sherehe ya siku ya wanawake kwa Kata ya Katandala
Sumbawanga.
Picha ya Pamoja kati ya viongozi wa Kata ya Katandala na wanawake waliohudhuria katika siku ya wanawake.
Picha
ya pamoja kati ya Watoto wa kituo cha Bethania na wanawake waliopeleka mahitaji
mbalimbali kwa watoto hao.
Afisa
Maendeleo ya Jamii Bi. Shukrani Sijaona akitoa mafunzo kuhusu ujasiliamali kwa
wanawake waliohudhuria katika sherehe ya siku ya wanawake katika kata ya
Katandala Sumbawanga
Diwani
wa Kata ya Katandala Mhe. Edwin Misasi akifungua mafunzo kwa wanawake
waliohudhuria katika sherehe ya siku ya wanawake katika kata ya Katandala
Sumbawanga.
Mheshimiwa
Deontina Kashaija akizungumza kwaniaba ya wanawake wakati wanakabidhi mahitaji kwa watoto wa kituo cha bethania.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni