Jumanne, 3 Machi 2026

WATUMISHI WASHAURIWA KUKOPA NBC KWAKUWA INA MASHARTI NAFUU

Na. Hilary Lorry – Mahakama, Lindi

Watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi wameombwa kuchukua mikopo katika Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa sababu benki hiyo imeingia Mkataba maalumu na Mahakama ya Tanzania kutoa mikopo hiyo kwa riba nafuu.

Taarifa hiyo ilitolewa hivi karibuni wakati wa Mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi baina ya wataalam kutoka Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) na watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi na Wilaya ya Lindi.

Akizungumza wakati wa Ufunguzi wa kikao hicho Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Consolata Peter Singano alisema kuwa, Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia mkataba maalum na Mahakama ya Tanzania juu ya utoaji wa Mikopo yenye masharti nafuu kwa watumishi wa Mahakama ya Tanzania.

Mhe.Singano aliwataka watumishi wa Mahakama hizo kuchangamkie fursa hiyo ya mikopo yenye masharti nafuu kwaajili ya kufanyia shughuli za maendeleo, kuliko kuchukua mikopo kwenye taasisi za fedha zenye riba kubwa.

Naye, Meneja wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Tawi la Lindi, Bw. Iovan Mapunda wakati wa uwasilishaji wa mada katika mkutano huo alisema kwamba Benki hiyo ilianzishwa rasmi Mnamo mwaka 1967 huku akipambanua kuwa benki hiyo ina hazina kubwa ya historia katika upande wa utoaji wa huduma bora za kibenki hapa Tanzania, pia akieleza kuwa benki hiyo ina bidhaa (products) nyingi za huduma kwa wateja wake.

Aidha, Meneja huyo alisisitiza kuwa endapo Mtumishi wa Mahakama ataamua ku pitisha mshahara wake benki ya NBC atapata Mkopo kwa asilimia 14 badala ya asilimia 17 ambazo zimezoeleka na zinazoonekana katika mfumo wa watumishi portal (ess),vilevile alieleza kuwa mkopo huo unaenda hadi miaka 65 kwa watumishi wa kawaida na miaka 80 kwa Majaji  na yote hayo ni kutokana na Mkataba maalum ulioingiwa kati ya benki hiyo na Mahakama ya Tanzania.

Kwa upande wake, Afisa Uhusiano kutoka Makao Makuu ya Beki hiyo Bw. Peter Mwasomola, aliongeza kuwa benki hiyo inatoa mikopo maalum kwa kuwakopesha watumishi wa Mahakama fedha kwa ajili ya kununua hati fungani za Serikali.

Vilevile, aliongeza kuwa, benki hiyo inatoa mikopo ya haraka (Chap chap loan) kupitia simu ya Mkononi yaani Salary Advance hadi asilimia 50 ya mshahara wako na kikubwa zaidi unaweza kuchukua mkopo huo kwa muda wa hadi miezi 12.

 Bw. Mwasomola aliwataka watumishi wa Mahakama ya Tanzania kufika katika ofisi za NBC kuchukua mikopo hasa ya muda mrefu ili kuitumia katika shughuli zao za maendeleo. “Kukopa siyo kubaya ila kukopa bila malengo ndiyo kubaya” alisistiza Bw. Mwasomola.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe.Consolata Peter Singano (aliyefunga kilemba katikati) akitoa neno wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo.

Watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi na Wilaya ya Lindi wakifuatilia mada zilizowasilishwa na wataalamu wa fedha kutoka benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa umakini Mkubwa.

Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bi.Quip Godfrey Mbeyela akitoa neo la utangulizi na ukaribisho kwa wataalamu kutoka Benki ya Taifa ya Biashara na Watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi na Wilaya ya Lindi.

Watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi na Wilaya ya Lindi wakifuatilia mada zilizowasilishwa na wataalamu wa fedha kutoka benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa umakini Mkubwa.

Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya ya Lindi Mhe. Khalfan O. Khalfan  akichangia mada katika mkutano huo.

Meneja wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) tawi la Lindi  Bw. Iovan Mapunda aliyenyoosha mkono akifafanua jambo wakati wa mkutano uliowakutanisha benki ya NBC na watumishi wa Mahakama ya Lindi.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni