Alhamisi, 5 Machi 2026

TANZIA

Bi. Lightness Elia Kiula wakati wa uhai wake.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Dar es Salaam Kisutu inasikitika kutangaza kifo cha Ofisa Tawala Mwandamizi, Bi. Lightness Elia Kiula, aliyekuwa akihudumu katika Mahakama ya Wilaya Kigamboni.

Kwa mujibu wa Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Bi. Athanasia Kabuyanja, kifo hicho kimetokea tarehe 04 Machi, 2026 katika Hospitali ya Moyo ya Jakaya (JKCI) iliyopo Upanga Dar es Salaam.

Bwana ametoa, Bwana ametwaa, Jina Lake lihimidiwe. Amen.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni