Jumatano, 1 Aprili 2026

JAJI MFAWIDHI MTWARA AFANYA UKAGUZI WA MAHAKAMA

Na SOJO STEPEHEN-Mahakama, Mtwara

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara, Mhe. Edwin Kakolaki, amefanya ziara ya ukaguzi wa Mahakama za Mkoa wa Mtwara ili kujionea utendaji kazi, hasa katika Mahakama za ya chini na kati kuhakikisha huduma ya utoaji haki inaendelea kufanya vyema.

Ziara hiyo ilifanyika tarehe 23 mpaka 25, Machi 2026. Miongoni mwa Mahakama zilizokaguliwa na ni Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mahakama za Wilaya Tandahimba, Newala, Nanyumbu, Masasi, Mahakama za Mwanzo Makuta, Mkunya, Mchaulo na Lukuledi.

Ziara hiyo pia ilijumuisha mazungumzo ya pamoja na Watumishi wa Mahakama alizopita kwa ajili ya ukaguzi. Aliweza kupata taarifa za utendaji kazi, mafanikio, changamoto, mapato na matumiz.

Aidha, Jaji Mfawidhi pia alipokea mawazo na maoni kutoka kwa Watumishi wa Mahakama hizo na kuhimiza weredi wa kuihudumia jamii inayowazunguka.

Mhe. Kakolaki aliwapongeza Mahakimu na Watumishi wa Mahakama kwa utendaji bora na mzuri, hasa kumaliza mashauri kwa wakati, kutokuwa na mlundikano na kuwa na aina bora ya utunzaji kumbukumbu.

Katika ukaguzi huo pia, Jaji Mfawidhi aliwapongeza Watumishi wa Mahakama katika matumizi wa mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ambayo inawezesha kufuatilia na kusikiliza mashauri kwa njia ya mtandao. Aliwasisitiza kuendelea kuwaelewesha Wananchi kwenye matumizi ya mifumo hiyo ili kupunguza gharama za kila mara.

Katika ziara hiyo, Jaji Mfawidhi aliambatana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara, Mhe. Seraphine Nsana, Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Kanda ya Mtwara, Bw. Yusuph Msawanga na Msaidizi wa Sheria wa Jaji Mfawidhi, Mhe. Stella Shindika

Jaji Mfawidhi pia alitembelea na kukagua Mahakama za Mwanzo zilizokuwa katika ujenzi na zile ambazo zilizokuwa tayari zimekamilika. Aidha, aliendelea kusisitiza ujenzi ufanyike kwa kuzingatia ubora na kwenda kwa wakati.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara, Mhe. Edwin Kakolaki akipokelewa na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Newala.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara, Mhe. Edwin Kakolaki, (wa tano kulia) katika picha ya pamoja na Watumishi alipotembelea Mahakama ya Mwanzo Mahuta Wilaya ya Tandahimba.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mwanzo Mkunya Wilaya ya Newala Mhe. Apatesile Mbalasila(kushoto), akisoma taarifa fupi ya Mahakama hiyo mara baada ya kumkaribisha Jaji Mfawidhi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara, Mhe. Edwin Kakolaki (kushoto) akiwa na Mhe. David Msalilwa(katikati), Mhe Charles Mnzava (kulia) katika mazungumzo na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Tandahimba.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara, Mhe. Edwin Kakolaki akitembelea Mahakama ya Mwanzo Mchauru.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara, Mhe. Edwin Kakolaki akiwa anakagua jengo la Mahakama ya Mwanzo Mchauru, ambalo lilipata maafa na kusababisha uharibifu.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara, Mhe. Edwin Kakolaki akikagua ujenzi wa jengo la Mahakama ya Wilaya Masasi.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara, Mhe. Edwin Kakolaki katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Nanyumbu.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni