Na. Iman Mzumbwe – Mahakama, Songwe
Mahakama
Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Songwe imefanya kikao cha Baraza la wafanya
kazi kilicholenga kujadili maswala muhimu ya kiutumishi, kuimarisha utendaji kazi
na kutunza maadili ya kiutumishi miongoni mwa watumishi.
Kikao
hicho kimefanyika tarehe 10 Aprili, 2026 katika Ukumbi wa Mahakama ya Hakimu
Mkazi Songwe, ambapo kiliongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Songwe
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Songwe Mhe. Gabriel Pascal Malata na kuwakumbusha
watumishi kutunza maadili na uwajibikaji kazini na mshikamano mahala pa kazi.
Mhe.
Malata alifungua kikao na kusoma ajenda mbalimbali ambazo ziliambatana na
uchaguzi wa viongozi waliopendekezwa na wajumbe wa Baraza la wafanya hilo
ambapo walipigiwa kura, huku wasimamizi wa uchaguzi huo wakiwa ni Katibu wa
Tughe Mkoa wa Songwe Bi. Magreth Emmanuel Mwantebwa na Afisa kazi Mkoa wa
Songwe Bi. Pendo Eva Lugendo.
Mhe.
Malata alitumia kikao hicho alitoa neno la shukurani kwa viongozi na wajumbe wa
Baraza la wafanyakazi Songwe walioshiriki katika kikao hicho huku akisistiza
kuendelea kushirikiana katika kutekeleza majukumu yao mahala pa kazi.
Vilevile,
Mhe. Malate aliwahimiza Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania
(TUGHE), viongozi wa matawi Tughe pamoja na viongozi wa Mahakama kuendelea kuwasisistiza
watumishi kujiunga na chama cha Tughe mahala pa kazi kwani chama hicho ni
muhimu na ni kwa mujibu wa sharia za vyama kazini. lakini pia ni muhimu kwa
sababu ya kutatua changamoto za watumishi na kutetea stahiki za watumishi kwa ujumla.
Aidha,
wajumbe wa Baraza hilo walipata fursa ya kuwasilisha hoja na mafanikio
waliyoyapata katika kipindi kilichopita, changamoto zinazowakabiri watumishi
pamoja na mikakati ya kuboresha mazingira ya kazi.
Sehemu
ya changamoto zilizowasilisha ilikuwa pamoja na uhitaji wa mafunzo endelevu kwa
watumishi wa Mahakama kwani kumekuwa na
maendeleo ya teknolojia inayohitaji mafunzo ili kuweza kuendana na mifumo
mbalimbali ya utendaji kazi kwa watumishi.
Baraza
hilo lilisisitiza umuhimu wa kuzingatia miongozo ya utumishi wa umma na sheria
zinazosimamia utendaji kazi, wajumbe walihimizwa kudumisha mshikamano na
kuheshimiana kazini ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu.
Kikao
hicho kilihudhuliwa na wajumbe kutoka Mahakama ya Mkoa Songwe na Mahakama za
wilaya kama vile Mbozi, Momba, Ileje, Songwe na Wengine walikuwa ni Katibu wa
TUGHE Mkoa Songwe Bi. Magreth Emmanuel Mwantebwa na Afisa kazi Mkoa wa Songwe
Bi. Pendo Eva Lugendo.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Gabriel Pascal Malata na Mwenyekiti wa kikao hicho cha Baraza la wafanya kazi (kushoto) akiwa Meza Kuu na Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Songwe Bw. Sostenes Mayoka (kulia) wakifuatilia kwa karibu shughuli za Baraza kwenye kikao hicho.
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Songwe Mhe. Gabriel Pascal Malata na Mwenyekiti
wa kikao hicho cha Baraza la wafanya kazi (katikati) akiwa katika picha ya
pamoja na katibu wa Baraza la wafanya kazi Mhe. Mesia Gang’olo (kulia) na Katibu
msaidizi Bi. Joyce Simba (kushoto) ambaye pia ni Msaidizi wa kumbukumbu katika
Mahakama ya Wilaya ya Momba - Songwe
Sehemu
ya wajumbe wa kikao cha Baraza la wafanya kazi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya
Songwe wakifatila kinachoendelea katika kikao hicho cha Baraza la wafanya kazi.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Songwe
Mhe. Gabriel Malata (hayupo pichani) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kikao wakiimba
wimbo wa mshikamamo.
Afisa
kazi Mkoa Songwe Bi. Pendo Eva Lugendo akikabidhi mkataba kwa Mwenyekiti wa
Baraza la wafanya kazi Songwe Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Songwe Mhe.
Gabriel Malata wakati wa kikao hichokilichofanyika katika katika ukumbi wa
Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni