Jumatatu, 13 Aprili 2026

MBEYA YAENDESHA BARAZA LA WAFANYAKAZI

Na. MWINGA MPOLI – Mahakama, Mbeya

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga ambaye ni Mweneyekiti Baraza la wafanyakazi Mahakama Kuu aliongoza watumishi wa Kanda hiyo kuendesha baraza hilo katika kujadili mambo mbalimbali yanayohusu watumishi ili kuendelea kujenga umoja, maadili na mshikamano mahali pa kazi.

Akiongea katika kikao hicho kilichofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano Mahakama Kuu Mbeya. Mwenyekiti huyo wa Baraza alisema, umuhimu wa kikao hicho ni kujadili dira ya taasisi kimkoa, kikanda na kuelezea muelekeo wa utekelezaji wa majukumu kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

“Nawaomba wajumbe kuwa wawazi katika kutoa Mawazo ya kujenga taasisi, mkikumbuka kwamba mnawawakilisha watumishi zaidi ya 300 katika kikao hiki lakini pia mkawe mabalozi wa kuwasilisha yale yote yaliyojadiliwa hapa,” alisema Mhe. Tiganga,

Kikao hiki kulihudhuriwa na Maafisa wawili kutoka TUGHE na wajumbe mbalimbali kutoka Mahakama kwa mujibu wa Mkataba mpya wa Baraza la wafanyakazi wa Mahakama.

Aidha katika kikao hicho pia kulifanyika uchaguzi wa kuwachagua Viongozi ambao ni Katibu na Katibu Msaidizi wa Baraza la wafanyakazi wa Mahakama Mkoa wa Mbeya na uchaguzi wa wajumbe wawakilishi wawili wa baraza kuu Taifa kufuatia wale waliokuwepo muda wao kuisha.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga (kushoto) akiongoza kikao hicho cha Baraza na kulia ni Katibu wa Baraza la wafanyakazi Mahakama Mkoa wa Mbeya Bw. Alintula Ngalile.

Katibu wa Baraza la wafanyakazi Mahakama Mkoa wa Mbeya Bw. Alintula Ngalile akielezea jambo katika kikao hicho.


Sehemu ya wajumbe katika kikao hicho

Sehemu ya wajumbe katika kikao hicho

Sehemu ya wajumbe katika kikao hicho

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga (katikati) kulia ni Afisa kutoka Tughe (aliyesimama) kushoto ni Katibu wa Baraza la wafanyakazi Mahakama Mkoa wa Mbeya Bw. Alintula Ngalile.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni