Na KANDANA LUCAS-Mahakama, Musoma
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Musoma, Mhe. Fahamu Mtulya, amewaongoza
wajumbe wa menejimenti kutembelea mapori ya akiba Ikorongo na Grumeti yaliyopo
katika Hifadhi ya Wanyama Serengeti kwa ajili ya kufanya utalii.
Ziara
hiyo ilifanyika baada ya kuhitimisha kikao cha menejimenti kilichofanyika mwishoni mwa mwezi
Machi 2026. Ziara hiyo pia ililenga kuwapa fursa wajumbe na Watumishi wengine
wa Mahakama kupata mapumziko mafupi na kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu
uhifadhi wa Wanyamapori.
Katika ziara hiyo, wajumbe waliweza kutembelea maeneo yenye Wanyama mbalimbali na walipatiwa elimu kuhusu uhifadhi na namna Wahifadhi wanavyokabiliana na changamoto za ujangili.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Musoma, Mhe. Fahamu Mtulya (mwenye
kofia) na Mtendaji wa Mahakama Kanda ya Musoma, Bw. Leonard Maufi, wakionesha
kundi la Wanyamapori (hawapo pichani).
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Musoma, Mhe. Fahamu Mtulya akiwaongoza
wajumbe wa menejimenti kufanya utalii wa kupanda mlima.
Kundi
la Nyati wakiwa kwenye moja ya mapori ya akiba katika hifadhi ya Wanyama
Serengeti.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Musoma, Mhe. Fahamu Mtulya (katikati
mwenye kofia mstari wa mbele) akiwa na Viongozi
wa mapori ya akiba Ikorongo na Grumenti pamoja na wajumbe wa menejimenti.
Meneja
Mahusiano kutoka Grumeti Fund, Bw. David Mwakipesile, akitoa elimu ya uhifadhi
wa Wanyamapori kwa wajumbe wa menejimenti (hawapo pichani).
Picha
za wanyama Simba akiwa porini, mmoja akiwa juu ya mti huku mwingine akitembea.
Picha
ya wajumbe wakiwa kwenye magari ya watalii.
Naibu
Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Musoma, Mhe. Monica Ndyekobora, akitoa neno kwa
wajumbe wa menejimenti (hawapo pichani) wakati wa ziara ya utalii.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni