Jumapili, 12 Aprili 2026

SUMBAWANGA YAFANYA KIKAO CHA MENEJIMENTI KUJADILI UTENDAJI KAZI

Na. SHARIFU MOKIWA- Mahakama, Sumbawanga

Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga ilifanya Kikao cha Menejimenti tarehe 10 Aprili, 2026 kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya kiutendaji na kuimarisha utoaji wa huduma za haki kwa wananchi.

Kikao hicho kilifunguliwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga Mhe, Frederick Manyanda ambaye aliwakaribisha Wajumbe kushiriki kikamilifu katika majadiliano kwa lengo la kuboresha utendaji wa Mahakama Kanda hiyo.

Aidha, katika Kikao hicho Mtendaji Mkuu Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu Essaba alisoma Muhtasari wa kikao ulifanyika tarehe 2 Aprili 2025 na kupitishwa rasmi na wajumbe ambapo uliidhinishwa kusainiwa.

Hata hivyo Wajumbe walipitia utekelezaji wa maazimio yatokanayo na Kikao kilichopita ambapo mambo mbalimbali yalijadiliwa kwa kuzingatia agizo la kikao hicho.

Pia taarifa hiyo ya utekelezaji 2025/2026 iliwasilishwa Mtendaji ikionyesha hali ya raslimali watu, maendeleo ya kiutendaji pamoja na utekelezaji wa majukumu mbalimbali.

Aidha, baada ya uwasiliswaji wa taarifa hiyo wajumbe walijadili masuala mbalimbali ya kiutendaji kwa lengo la kuboresha utendaji kazi, usimamizi wa raslimali na utoaji huduma kwa wananchi 

Kupitia Kikao hicho Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga Mhe. Frederick Manyanda aliunda Kamati ya watu wa watano ambao ni Naibu Msajili, Afisa TEHAMA, Hakimu Mkazi Mfawidhi, Msaidizi wa Kumbukumbu mmoja na Mwandishi mwendesha ofisi mmoja kwa ajili ya kushughulikia yale maeneo ambayo utekelelezaji wake ni hafifu.

Kwa upande wake, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga Mhe. Thadeo Mwenempazi aliwasisitiza Mahakimu wa Mahakama za Wilaya wanapopokea rufaa kutoka Mahakama za Mwanzo wawe wanaingiza kwenye mfumo wa e-CMS taarifa za majalada yaliyotoka Mahamaka za Mwanzo kama vile mienendo ya mashauri (proceedings), nakala za hukumu pamoja na vielelezo ili kurahisisha utendaji kazi.

Kikao hicho kilihitimishwa kwa wito kwa wajumbe kuhakikisha utekelezaji wa maamuzi yaliyofikiwa unafanyika kwa wakati na ufanisi ili kuimarisha utoaji wa haki kwa wananchi.



Mtendaji Mkuu Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu Essaba alisoma Muhtasari wa kikao cha menejimenti na taarifa ya utekelezaji 2025/2026.

Sehemu ya wajumbe wa kikao cha menejimenti wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga 

Mjumbe wa kikao Bw. Mayanga Someke akichangia hoja katika Kikao cha Menejimenti 



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni