Na SHARIFU MOKIWA, Mahakama-Sumbawanga
Mahakama
Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga ilifanya kikao cha watumishi chenye lengo
la kuwatambulisha watumishi wapya pamoja na kutoa maelekezo ya kuboresha
utendaji kazi wa utoaji huduma kwa wananchi.
Kikao
hicho kilichofunguliwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe.
Frederick Manyanda na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Jaji wa
Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Thadeo Mwenempanzi, Mtendaji wa Mahakama Kuu,
Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu Essaba, Naibu Msajili Mahakama Kuu, Kanda ya
Sumbawanga Mhe. Pamela Mazengo pamoja na Watumishi wa Mahakama.
Akizungumza
katika kikao hicho, Mhe. Manyanda aliwakaribisha watumishi wapya waliopangiwa
kufanya kazi Mahakama Kanda ya Sumbawanga kutoka maeneo mbalimbali ya nchi
akisisitiza umuhimu wa kuzingatia kanuni na maadili ya utumishi wa Umma.
Alieleza
kuwa, kila mtanzania ana haki ya kuishi na kufanya kazi popote nchini ilimradi
anazingatia sheria na taratibu, huku akiwahimiza watumishi kupenda maeneo yao
ya kazi na kuyachukulia kwa mtazamo chanya. “Tanzania ni nchi yetu sote kila
mtu ana haki ya kuishi mahali popote ilimradi havunji sheria za nchi.” Amesema Mhe.
Manyanda.
Aidha,
Mhe. Manyanda alisisitiza uwajibikaji, uadilifu na weledi na pia kujiongeza (Proactivity)
katika utekelezaji wa majukumu pamoja na umuhimu wa kujifunza na kujiendeleza
kitaaluma.
Naye,
Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu Essaba aliwasilisha
mrejesho wa kikao cha bajeti kilichofanyika tarehe 16 hadi19 Februari, 2026 kilichofanyika
Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.
Bw.
Essaba alieleza kuwa, rasilimali fedha ni chache hivyo matumizi yake yanapaswa
kuzingatia vipaumbele vilivyowekwa ili kuhakikisha shughuli za Mahakama
zinaendelea kwa ufanisi.
Aidha,
alisisitiza umuhimu wa ushurikiano wa karibu katika utendaji kazi kati ya Mtendaji
na Naibu Msajili katika kuimalisha utekelezaji wa majukumu ya kimahakama. “Naibu
Msajili ni injini ya utekelezaji wa majukumu ya kimahakama katika Kanda,” aliongeza
Mtendaji huyo.
Bw.
Essaba alisema kuwa, masuala ya kiutawala ikiwemo usimamizi wa matumizi ya
fedha kwa kuzingatia bajeti, matengenezo na usalama wa magari ya Mahakama, na
utunzaji wa mazingira ya ofisi, vilevile alikumbusha umuhimu wa nidhamu ya
mahudhurio kazini, ambapo kutosaini siku tano mfululizo huhesabika kama utoro.
Vilevile,
Bw. Essaba alitumia fursa hiyo kumkaribisha Naibu Msajili mpya wa Mahakama Kuu
Kanda ya Sumbawanga Mhe. Pamela Mazengo aliyehamia kutoka Mahakama Kuu Kanda ya
Tabora ili kuchukua nafasi ya Mhe, Joseph Luambano aliyehamia Mahakama Kuu, Kanda
ya Njombe.
Mara
baada utambulisho huo Mhe. Mazengo alisema kuwa, amekuja kujifunza, kushirikiana
na watumishi katika kuhakikisha utoaji wa haki kwa wananchi unafanyika kwa
ufanisi. “Nimekuja kujifunza na kushirikiana nanyi tusimame pamoja katika
jukumu la kutenda haki kwa wateja wetu kwa upendo.”
Kwa
upande wake, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe, Thadeo Mwenempazi aliwakumbusha
watumishi wapya kuwa ajira ni jukumu la mtu binafsi na kila mtumishi anapaswa
kuwajibika kikamilifu katika nafasi yake. Alisisitiza matumizi ya muda na
umuhimu wa kujifunza kwa bidii ili kujenga msingi mzuri wa maisha ya baadae.
Katika
hatua nyingine Jaji mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Manyanda
aliwasilisha tuzo aliyopokea kama pongezi na shukrani kutoka Mahakama Kuu Kanda
ya Katavi kama kielelezo cha mchango wake katika kuisimamia na kuilea Mahakama
hiyo hadi kufikia hatua ya kujitegemea kiutendaji.
Jaji
Mfawidhi Mahakama ya Sumbawanga Mhe. Frederick Manyanda (aliyesimama) akitoa nasahaa kwa
watumishi wapya kuhusu uwajibikaji, maadili na utumishi bora. Wengine ni
Jaji
wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe.Thadeo Mwenempazi akizungumza neno wakati
wa kikao cha watumishi.
Mtendaji
wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu Essaba akiwasilisha mrejesho wa
kikao cha bajeti na kusisitiza mtumizi sahihi ya rasilimali za umma.
Naibu
Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Pamela Mazengo akizungumza
baada ya kutambulishwa rasmi mbela ya watumishi.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Frederick Manyanda akizindua Kitabu
cha Utendaji kazi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga kwa mwaka 2025.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Frederick Manyanda akiwasilisha tuzo aliyopokea kama pongezi na shukrani kutoka Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Katavi kwa mchango wake katika kuisimamia na kuilea Kanda hiyo.
Watumishi
wapya wa Mahakama waliosimama wakati wa utambulisho ili kutengeneza namna bora ya kuwajengea
uelewa wa pamoja wa majukumu yao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni