Na FRANCISCA SWAI – Mahakama, Musoma.
Mahakimu, Waendesha
Mashtaka na Maofisa Ustawi wa jamii jana tarehe 13 Aprili, 2026 walipatiwa
mafunzo ya namna ya kuepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa
kingono kabla ya kesi, wakati wa kutoa ushahidi mahakamani na baada ya kesi.
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu, Kanda ya Musoma, Mhe. Marlin Komba, akifungua mafunzo hayo yanayotolewa katika
ukumbi wa Mahakama Kuu Kanda ya Musoma, alisema mafunzo haya ni mahsusi kwa
ajili ajili ya kuwajengea uwezo washiriki katika kushughulikia mashauri ya
ukatili wa kijinsia kwa kuzingatia athari mbalimbali wanazopata wahusika, hasa
za kiakili na kihisia.
Aidha, Mhe. Komba
alisisitiza umuhimu wa washiriki hao kutumia weledi, lugha zenye huruma na
staha pamoja na mbinu rafiki katika shughulikia mashauri ya unyanyasaji ili
kutowajengea waathirika woga au kumbukumbu mbaya kutokana na majeraha
waliyokwisha yapata hapo awali.
Mafunzo hayo ya siku tatu
yatagusa maeneo mbalimbali, ikiwemo ushirikiano baina ya Taasisi katika
kuwasaidia mashahidi walioko katika mazingira magumu, uelewa wa athari za
kiakili na kihisia kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia pamoja na mbinu rafiki
na salama za kuuliza maswali ili kuhakikisha utu na hisia za waathirika
zinalindwa kuwaondolea woga wanapokuwa wakitoa ushahidi mahakamani.
Washiriki wa mafunzo hayo wametoka Wilaya za Simiyu, Maswa, Meatu, Busega, Sengeti, Tarime, Bunda, Rorya, Bariadi na Itilima.
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda yaMusoma, Mhe. Marlin Komba akifungua mafunzo hayo kwa Mahakimu, Waendasha Mashtaka, Maofisa Ustawi wa Jamii yaliyohusu uwezo kuepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kingono.
Hakimu Mkazi na Mratibu
wa mafunzo kutoka Chuo cha uongozi wa Mahakama (IJA), Mhe. Gloria Shuma,
akiwakaribisha washiriki wakati wa ufunguzi wa mafunzo haya.
Naibu Msajili wa Mahakama
Kuu Musoma, Mhe. Omary Kingwele (aliyesimama), akitoa neno wakati wa ufunguzi
wa mafunzo hayo.
Mwezeshaji, Mhe, Venance
Mlingi (aliyesimama mbele) akielezea na kusisitiza jambo wakati wa mafunzo
hayo.
Sehemu ya washiriki wa
mafunzo hayo wakifuatilia kwa umakini mada mbalimbali zinazoendelea kutolewa na
wawezeshaji.
Ofisa
Ustawi wa Jamii, Bi. Consolata Makomelo (aliyesimama) akiwasilisha mada wakati
wa mafunzo hayo.
Muwezeshaji katika
mafunzo hayo, Mhe, Nabwike Mbaba (aliyesimama) akiwasilisha mada kuhusiana na
atahari za ukatili wa kinsia na kingono.
Wawezeshaji pamoja na
washiriki wa mafunzo wakimsikiliza Mwananchi ambaye ndio mara yake ya kwanza
kuingia mahakamani, Bi. Elizabeth Roman (aliyesimama kizimbani) aliyeshiriki
katika igizo fupi, akielezea uzoefu alioupata kupitia tukio hilo ikiwa ni
sehemu ya tathmini ya kujua namna waathirika wa matukio ya ukatili wavyojisikia
wakati wa uendeshaji wa mashauri hayo.
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Marlin Komba (katikati), Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Omary Kingwele (kushoto), Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Monica Ndyekobora (kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji wa mafunzo hayo, Mhe. Venance Mlingi (aliyesimama kushoto) na Mhe. Nabwike Mbaba (aliyesimama kulia).
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Marlin Komba (katikati), Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Omary Kingwele (kushoto), Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Monica Ndyekobora (kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wote wa mafunzo hayo.
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Marlin Komba (katikati), Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Omary Kingwele (kushoto), Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Monica Ndyekobora (kulia), akiwapamoja na sekretariet ya mafunzo hayo, Mhe. Gloria Shuma (aliyesimama kulia) na Mhe. Prisca Mkeha (aliyesimama kushoto).
Habari hii imeharriwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.










Hakuna maoni:
Chapisha Maoni