Na MWANDISHI WETU-Mahakama, Dodoma
Aliyekuwa Dereva wa Mahakama ya Tanzania, Makao
Makuu Dodoma, Iddi Nassibu Chumu, ambaye alifariki dunia tarehe 23 Mei, 2026, alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma (General
Hospital), amepumzishwa kwenye nyumba yake ya milele.
Marehemu Chumu amezikwa kwenye makaburi katika Wilaya ya
Kisarawe mkoani Pwani, tukio lililohudhuriwa na mamia ya Wananchi, wakiwemo
Watumishi w Mahakama ya Tanzania, na kuacha simanzi kubwa.
Ifuatayo ni sehemu ya matukio katika picha ya maziko hayo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni