Na. ALLY RAMADHANI – Mahakama, Katavi.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Katavi, Mhe. Godfrey
Ntemi Isaya amewasisitiza watumishi wa Mahakama za Mwanzo katika Masjala hiyo
kutumia Mifumo ya TEHAMA katika shughuli zao za kiutendaji.
Hayo
yalisemwa hivi karibuni na Mhe. Isaya alipokuwa kwenye ziara yake ya ukaguzi wa
Mahakama ili kuangalia utendaji kazi wa kila siku wa utoaji huduma za haki kwa
wananchi, ziara hiyo ya ukaguzi ilifanyika kuanzia tarehe 28 Aprili, 2026 hadi
07 Mei 2026 katika Wilaya za Mpanda, Mlele na Tanganyika.
Katika
ziara hiyo, Mhe. Isaya alifanikiwa kutembelea Vituo vyote vya Mahakama za
Mwanzo zinazoendelea kujengwa ndani ya Mkoa wa Katavi kama vile Sibwesa, Ugalla
na Mamba na kupata wasaa wa kuwasisitiza watumishi wa maeneo hayo kuendeleza na
mapambano ya matumizi ya TEHAMA ili kurahisisha utoaji haki kwa wananchi
wanaowahudumia.
Kupitia
ziara hiyo Mhe. Isaya aliwakumbusha watumishi wa Mahakama za Mwanzo mkoani
Katavi kuendelea kutumia Mifumo ya TEHAMA ikiwemo Primary Court App, ili kurahisha
utendaji kazi wa Mahakama kwa ujumla.
Aidha,
Mhe. Isaya aliongeza kuwa, kazi ya kutoa haki sio jambo dogo hivyo watumishi
wasijiingize katika vitendo viovu vinavyoweza kuharibu taswira ya Mahakama na
kupunguza imani kwa wananchi,
“Ndugu
watumishi nawasisitiza kuwa waadilifu kwa kuwa ndiyo msingi mkubwa wa kutoa
haki, hivyo muwe na tabia njema kazini na nje ya kazi na tuendelee kuchapa kazi
tuwatumikie wananchi, tuepuke ile hali ya kuwa miungu watu kwenye ofisi zetu na
kuongeza kuwa, kila mmoja kufanya kazi kwa bidii na umoja “If people cannot pay you, the
nature will,” alisema Jaji Isaya.
Kwa
upande mwingine, Mhe Isaya aliwapongeza watumishi wote kwa ujumla kwa kazi
nzuri inayofanyika hususani usikilizwaji wa mashauri kwani katika taarifa zote
zilizowasilishwa zimeonyesha kuwa mashauri yanafunguliwa na yanaisha kwa
wakati.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Katavi Mhe. Godfrey Ntemi Isaya (katikati) akiwa kwenye Picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Masjala hiyo alipotembelea jengo la Mahakama ya Mwanzo Wilaya Mpanda Kituo cha Ugalla.
Naibu Msajili Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Katavi,
Mhe. Silivia S. Lushasi (aliyesimama) akiongea na watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Wilaya
Mpanda kituo cha Mpanda Mjini alipokua kwenye ziara ya Mhe Jaji Mfawidhi Kanda
ya Katavi.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo
ya Katavi Mhe. Godfrey Ntemi Isaya (wa kwanza Kulia mwenye suti
nyeusi) akikagua baadhi ya mipaka ya eneo la Mahakama ya Mwanzo Wilaya Mpanda Kituo
cha Shanwe.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni