Na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa Majaji tisa
wa Mahakama Kuu kuwa Majaji wa Mahakama ya Rufani.
Taarifa iliyotolewa na
Mkurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, Bw. Bakari Machumu, leo tarehe 20 Mei,
2026, imesema kuwa wateule hao wataapishwa tarehe itakayotangazwa baadaye.
Walioteuliwa ni Majaji saba
wa Mahakama Kuu ya Tanzania na wengine wawili kutoka Mahkama Kuu ya Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa
iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, walioteuliwa
ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Dodoma, Mhe. Abdi Shaaban
Kagomba na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Arusha, Mhe. Yohane Bokobora
Masara.
Wengine ni Jaji Mfawidhi
wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Bukoba, Mhe. Immaculata Kajetan
Banzi na Jaji wa Mahkama Kuu ya Zanzibar, Mhe. Rabia Hussein Mohamed.
Wateule wengine ni Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Biashara, Dar es Salaam,
Mhe. Cyprian Phocas Mkeha na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni
ya Kazi, Dar es Salaam, Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina.
Wengine ni Jaji wa Mahakama
Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu Dodoma, Mhe. Iman, Daud Aboud, Jaji wa Mahkama
Kuu ya Zanzibar, Mhe. Mzee Ibrahim Ibrahim na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya
Tanzania, Masjala Ndogo Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Laurent Masabo.
Mhe. Yohane Bokobora Masara.
Mhe. Immaculata Kajetan Banzi.
Mhe. Rabia Hussein Mohamed.
Mhe. Cyprian Phocas Mkeha.
Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina.
Mhe. Iman, Daud Aboud.
Mhe. Mzee Ibrahim Ibrahim.









Hakuna maoni:
Chapisha Maoni