Na. MUKSINI NAKUVAMBA - Mahakama, Mbeya
Idara
ya Usimamizi wa Mashauri (DCM) ilifanya ziara katika Mahakama Kuu ya Tanzania
Masjala Ndogo ya Mbeya hivi karibuni kutathimini juu ya hali ya utoaji wa huduma
zitolewazo na Mahakama Inayotembea katika Masjala hiyo.
Katika
kikao kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Mahakama Kuu Masjala hiyo kikiongozwa
na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania kutoka Idara ya Usimamizi wa Mashauri
(DCM) Mhe. Moses Betwel Ndelwa, ili kujadili juu ya changamoto mbalimbali
wanazokumbana nazo katika utoaji wa huduma za Mahakama Inayotembea.
Aidha, Mhe. Ndelwa aliwasisitiza wasimamizi na
watumiaji wote wa gari la Mahakama Inayotembea (Mobile court Service)
kuzingatia misingi na taratibu za matumizi ya gari hilo.
“Matumizi
ya Gari la Mahakama Inayotembea (Mobile court Service) yazingatie huduma za Mahakama
Inayotembea tu na si vinginevyo,” alisisitiza Mhe. Ndelwa
Mhe.
Ndelwa aliongeza kuwa, usikilizwaji wa mashauri kwenye Mahakama Inayotembea
usizidi siku thelathini (30) tangu tarehe ya kufunguliwa kwa shauri. Sambamaba
na hilo aliwasisitiza watumishi wanaofanya kazi katika Mahakama Inayotembea
kufanya kazi kwa bidii na uadilifu na kuwa mfano wa kuigwa katika utoaji wa
huduma bora za kimahakama.
Vilevile,
Mhe. Ndelwa aliwashukuru Idara ya fundi sanifu, umeme, maji na TEHAMA Mahakama
Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya kwa kuwa mstari wa mbele katika kutatua changamoto
ndogo ndogo zinazojitokeza kwenye Gari la Mahakama Inayotembea na kupelekea
utendaji bora wa kazi.
Pia
aliwaasa Mahakimu Wafawidhi Mkoa na Wilaya ya Mbeya kufanya ziara za mara kwa mara
ili kufuatilia hali ya huduma zitolewazo kwenye Mahakama inayotembea.
Sambamba
na kikao hicho, ugeni huo ulifanya ziara ya ukaguzi wa miundombinu ya Gari
linalotoa huduma ya Mahakama inayotembea na kutembelea moja ya kituo cha
kutolea huduma za Mahakama inayotembea katika Kata ya Uyole ndani ya jiji la
Mbeya na kujionea Mazingira ya utolewaji wa huduma za Mahakama Inayotembea
kwa wananchi.
Mwenyekiti wa kikao, Naibu Msajili Mahakama ya Tanzania kutoka Idara ya Usimamizi wa Mashauri (DCM) Mhe. Moses Betwel Ndelwa (katikati) akizungumza katika kikao cha Tathmini ya utendaji kazi wa Mahakama Inayotembea, kulia ni Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Aziza Temu na kushoto ni Hakimu Mkazi Mwandamizi Mhe. Sifa Jacob.
Maafisa Mahakama kutoka
Idara ya Usimamizi wa Mashauri (DCM) wakiwa katika ziara ya kutembelea moja ya
kituo cha kutolea huduma ya Mahakama inayotembea (Mobile Court Service)
Maafisa Mahakama kutoka
Idara ya Usimamizi wa Mashauri (DCM) wakiwa katika ziara ya kutembelea moja ya
kituo cha kutolea huduma ya Mahakama inayotembea (Mobile Court Service)
Maafisa Mahakama kutoka
Idara ya Usimamizi wa Mashauri (DCM) wakiwa katika ziara ya kutembelea moja ya
kituo cha kutolea huduma ya Mahakama inayotembea (Mobile Court Service) wa kwanza
kulia ni Mtendaji wa Kata ya Uyole Bi. Sikuzani Kibona
Maafisa Mahakama kutoka Idara ya Usimamizi wa Mashauri
(DCM) na Viongozi wa Mahakama Kuu kutoka Masjala Ndogo ya Mbeya wakiwa kwenye picha
ya Pamoja na Watumishi wanaohudumu katika Mahakama inayotembea (Mobile Court
Service), Nyuma yao ni Gari linalotoa huduma ya Mahakama inayotembea likiwa
mbele ya jengo la mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya.
Sehemu ya washiriki wa kikao hicho cha tathmini.
Sehemu ya washiriki wa kikao hicho cha tathmini.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni