Na. MUKSINI NAKUVAMBA, Mahakama Mbeya
Naibu Msajili
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Aziza Temu
amefanya ziara ya kutembelea Gereza Kuu la Ruanda jijini Mbeya hivi karibuni kwa
ajili ya kusikiliza changamoto mbalimbali za wafungwa na Mahabusu wa Gereza
hilo, ikiwa ni zaira ya ukaguzi wa kawaida gerezani hapo katika kipindi cha
Aprili –Juni, 2026.
Akiwasilisha
taarifa fupi ya Gereza Kuu la Ruanda Mkuu wa Gereza Kamishna Msaidizi wa
Magereza ACP Christopher Fungo, alieleza hali za wafungwa na mahabusu waliopo gerezani
hapo.
Katika
ziara hiyo Mhe. Temu alipata fursa ya kukutana na Wafungwa na Mahabusu ambao
waliwasilisha changamoto zao kwa viongozi mbalimbali wa Mahakama na wadau
wengine wa haki jinai alioambatana nao katika ziara hiyo.
Katika
risala yao wafungwa na mahabusu waliweza kuwasilisha changamoto mbalimbali
zinazowakabili gerezani hapo. Aidha Mhe. Temu aliahidi kuzishughulikia
changamoto zote zilizowasilishwa katika risala zao na zile ambazo zipo nje ya
uwezo kuziwasilisha katika mamlaka husika.
Kwa
upande wake Mkuu wa Gereza Ruanda ACP Christopher Fungo alitoa shukurani zake
kwa ujio wa ziara hiyo, kwa kuwa umekuwa na tija kubwa kwao kwa kutoa fursa
kadhaa ikiwemo matendo ya huruma na kushughulikia suala la kupunguza mlundikano
wa mahabusu gerezani hapo.
Katika
ziara hiyo Mhe. Temu aliambatana na Viongozi mbalimbali wa Mahakama akiwemo Kaimu
Mtendaji Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya Bw. Alintula Ngalile, Mahakimu Wakazi
wakiongozwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Mhe. Zawadi
Laizer, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka (NPS), Mwenyekiti TLS Chapta ya Mbeya,
Maafisa wa TAKUKURU, Ofisi ya Upelelezi Mkoa wa Mbeya, Afisa Huduma na
Uangalizi Mbeya na wadau wengine wa Haki jinai.
Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya
Mbeya Mhe. Aziza Temu (wanne kulia) akiwa kwenye picha ya Pamoja na viongozi wa
Grezeza Ruanda na Mahakama kanda ya Mbeya na wadau wengine wa haki jinai
alioambatana nao mbele ya Lango la Gereza Kuu Ruanda Mbeya. watatu kulia ni
Mkuu wa Gereza Kuu Ruanda Mbeya Kamisha Msaidizi ACP Christopher Fungo, Hakimu
Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Mhe. Zawadi Laizer (watano
kulia), Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbeya, Mhe. Tedy Mlimba
(wapili kulia).
Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Aziza Temu (aliyeketi mbele) na wadau wengine wa haki jinai alioambatana nao katika ziara hiyo wakiwa ndani ya ofisi ya Mkuu wa Gereza la Ruanda Mbeya. Aliyesimama ni Mkuu wa Gereza Kuu la Ruanda Mbeya Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Christopher Fungo.
Viongozi wa Mahakama na Maafisa kutoka Taasisi mbalimbali za haki jinai walioshiriki katika ziara hiyo wakiwa Mbele ya kasha linalotoa huduma ya mahakama mtandao Gereza Kuu Ruanda
Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Aziza Temu (wa kwanza aliyeketi kushoto) na wadau wengine wa haki jinai alioambatana nao katika ziara hiyo wakiwa ndani ya ofisi ya Mkuu wa Gereza la Ruanda Mbeya. Aliyesimama ni Mkuu wa Gereza Kuu la Ruanda Mbeya Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Christopher Fungo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni