Na. REHEMA AWET – Mahakama, Mwanza
Mahakama
Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Mwanza imeingia katika awamu mpya ya Uongozi
leo tarehe 17 Juni, 2026, baada ya hafla ya makabidhiano ya Ofisi ya Jaji
Mfawidhi kufanyika.
Hafla
hiyo iliyofanyika katika Ofisi ya Jaji Mfawidhi Masjala Ndogo ya Mwanza, ilishuhudiwa
na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Dkt. Ntemi Kilekamajenga akikabidhi rasmi
kijiti cha uongozi kwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ephery Kisanya.
Makabidhiano
hayo yalijikita katika kukabidhi majukumu ya kiutawala, nyaraka mbalimbali za
ofisi, na taarifa muhimu za utendaji kazi, zote zikiwa na lengo la kuhakikisha
mwendelezo wa utoaji wa huduma za kimahakama na usimamizi wa shughuli za
Mahakama katika Masjala Ndogo hiyo ya Mwanza.
Akizungumza
katika hafla hiyo, Jaji Dkt. Ntemi Kilekamajenga alimpongeza Jaji Ephery
Kisanya kwa kukabidhiwa majukumu hayo na kumtakia mafanikio katika utekelezaji
wake.
Kwa
upande wake, Jaji Ephery Kisanya aliahidi kuendesha ofisi hiyo kwa weledi,
kuendeleza ushirikiano baina ya wafanyakazi, na kuimarisha upatikanaji wa
huduma za haki kwa wananchi wa Masjala hiyo ya Mwanza.
Makabidhiano
hayo yanaashiria mwanzo wa awamu mpya ya uongozi katika Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mwanza, huku yakisisitiza dhamira ya kuendeleza ufanisi, uwazi na ubora
katika utoaji wa huduma za Mahakama kwa wananchi.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni