Na. SHARIFU MOKIWA – Mahakama, Sumbawanga
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Sumbawanga Mhe. Frederick
Kapela Manyanda amefanya ziara ya kutembelea Gereza la Mahabusu Sumbawanga na
Gereza la Mollo la Kilimo kwa ajili ya kusikiliza changamoto mbalimbali za wafungwa
na Mahabusu wa magereza hayo, ikiwa ni zaira ya ukaguzi wa kawaida katika
kipindi cha Juni, 2026.
Akiwasilisha
taarifa fupi ya Gereza Kuu la Mahabusu Sumbawanga jana tarehe 15 Juni, 2026
Mkuu wa Gereza Mahabusu Sumbawanga Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Ally M. Abdallah
alieleza hali za wafungwa na mahabusu
waliopo gerezani hapo.
Mhe.
Manyanda alipata fursa ya kukutana na Wafungwa na Mahabusu ambao waliwasilisha
changamoto zao kwa viongozi mbalimbali wa Mahakama na wadau wengine wa haki
jinai alioambatana nao,
Akijibu
hoja mbalimbali Mhe. Manyara alielekeza kuharakishwa kwa hatua za upelelezi wa
mashauri mbalimbali yanayohusisha Watoto ili kuhakikisha haki inatendeka kwa
wakati mapema ipasavyo na wahusika wanapata huduma stahiki kwa mujibu wa
sheria.
Aidha,
Mhe. Mnyanda, alielekeza kubainishwa kwa changamoto zinazo kwamisha mwenendo wa
mashauri ya jinai na kuzitaka kamati za haki jinai kushirikiana kwa karibu
katika kuzitatua pamoja na kusukuma mbele mashauri yaliyopo ili kupunguza mlundikano
wa mashauri.
Katika
risala yao wafungwa na mahabusu katika Gereza la Mahabusu Sumbawanga waliweza
kuwasilisha changamoto mbalimbali zinazowakabili gerezani hapo mbele ya Mhe.
Manyanda. Aidha, Mhe. Manyanda aliahidi kuzishughulikia changamoto zote
zilizowasilishwa katika risala zao na zile ambazo zipo nje ya uwezo
kuziwasilisha katika mamlaka husika.
Kwa
upande wake, Mkuu wa Gereza la Mahabusu Sumbawanga ACP Ally M. Abdallah alitoa
shukurani zake kwa ujio wa ziara hiyo, kwa kuwa umekuwa na tija kubwa kwao kwa
kutoa fursa kadhaa ikiwemo matendo ya huruma na kushughulikia suala la
kupunguza mlundikano wa mahabusu gerezani hapo.
Katika
ziara hiyo Mhe. Manyanda aliambatana na Viongozi mbalimbali wa Mahakama akiwemo
Mtendaji Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Sumbawanga Bw. Machumu Essaba, Msaidizi wa Sheria, Mkuu
wa upelelezi Mkoa, Kaimu Hakimu Mkazi Mkoa, Hakimu Mfawidhi wa Wilaya, Afisa
Ustawi Mkoa, Mkuu wa Mashtaka Mkoa, Mwakilishi
wa Kamanda Takukuru Mkoa, Ofisi ya Upelelezi Mkoa, Afisa Huduma na Uangalizi, Afisa
Uhamiaji Mkoa, Mkuu wa Magereza Mkoa na wadau wengine wa Haki jinai.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Sumbawanga Mhe.
Frederick Kapela Mnyanda (katikati) akiwa pamoja na wadau wengingine wa
haki jinai wakiwa katika gereza la kilimo Mollo.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Sumbawanga Mhe. Frederick Kapela Manyanda
(kushoto) akipokea risala kutoka kwa Afisa wa Jeshi la Magereza.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo
Sumbawanga Mhe. Frederick Kapela Manyanda (mbele
ya picha kulia) akiwasili katika ukaguzi wa Gereza la Mahabusu Sumbawanga.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha-Mahakama)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni