Na. MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga
amesema ushirikiano na mahusiano mazuri kazini ni nyenzo muhimu katika
kuboresha utendaji kazi ujumbe huo ameutoa wakati alipotembelea Mahakama
zilizopo Mbeya Mjini ikiwa ni kuanza kwa ukaguzi wa kawaida warobo ya nne ya mwaka
2025/2026.
Ziara
hiyo iliyofanyika mwanzoni mwa mwezi Juni, kwa kutembelea sehemu ya Mahakama kwa
lengo la kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa katika Mahakama hizo na alipata
wasaa wa kuzungumza na watumishi wa Mahakama hizo katika vikao vya pamoja
vilivyofanywa wakati wa ziara hiyo.
Akizungumza
katika vikao hivyo, vilivyofanyika katika ukaguzi huo, Mhe. Tiganga alisisitiza
kudumisha nidhamu, ushirikiano na mahusiano mazuri mahala pa kazi ikiwa ni pamoja
na ushirikishwaji wa watumishi katika kupanga mambo mbalimbali ya kiutendaji.
“Nasisitiza
kudumisha nidhamu na mahusiano mazuri kazini, tuishi kwa upendo na tujifunze
kuvumiliana pale inapotokea kupishana baina yetu, tuepuke mambo ambayo hayana ulazima
Kutugawa, tusitengeneze ugumu wa kazi kwa kuwekeana vinyongo na vikwazo baina
yetu. Pia nawakumbusha kuhusu umuhimu wa ushirikishwaji wa watumishi katika
kupanga mambo mbalimbali ya kiutendaji katika ofisi zetu,” alisema Mhe. Tiganga
katika ziara yake hiyo.
Mhe.
Tiganga aliongezea kwa kusisitiza umuhimu wa kutunza na kulinda rasilimali za Mahakama
na kuzingatia hasa vipaumbele vya ofisi kulingana na bajeti zenu kila fedha za
matumizi ya ndani zinapoletwa.
Aidha Mahakimu Wafawidhi wa Vituo hivyo alivyotembelea walitoa shukrani zao kwa ziara hiyo na kuahidi kuwa wako tayari kutekeleza yale yote waliyoelekezwa na viongozi wao ili kuboresha utendaji kazi katika vituo vyao na kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Aidha,
kupitia taarifa mbalimbali zilizowasilishwa na Mahakimu Wafawidhi wa Vituo
mbalimbali alivyotembelea zilieleza juu ya usimamizi wa rasilimali mbalimbali
zilizopo, utekelezaji wa majukumu ikiwa ni pamoja na hali ya mashauri katika
vituo hivyo.
Sambamba
na hilo, Taarifa hizo zilieleza changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo katika
vituo vyao ambapo wengi wao walieleza hasa kuhusu uhaba wa watumishi hasa kada
ya walinzi, uchakavu wa vyombo vya usafiri na uchakavu wa majengo hasa kwa Mahakama
za mwanzo.
Katika
ziara hiyo Mhe. Tiganga, aliambatana na viongozi mbalimbali wa Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya, akiwemo Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi.
Mavis Miti, Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Judith
Lyimo, Afisa Utumishi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bw. Moses Luoga na Hakimu
Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Mhe. Zawadi Laizer.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya
Mhe. Joachim Tiganga (wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama ya
Watoto Mbeya.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya
Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (katikati) akiwa ndani ya Ofisi ya Mahakama ya
hakimu mkazi Mbeya, kulia ni Naibu Msajili Mahakama Kuu Majala Ndogo ya Mbeya
Mhe. Judith Lyimo na kushoto ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu
Mkazi Mbeya, Mhe. Zawadi Laizer.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga (katikati walioketi mbele). akiwa kwenye picha ya pamoja na
watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, walioketi mbele, kulia ni Mtendaji
wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti na kushoto ni Naibu Msajili
Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Judith Lyimo.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga (watatu kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa
Mahakama ya wilaya Mbeya katika ukaguzi huo, wanne kulia ni Hakimu Mkazi
Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbeya, Mhe. Tedy Mlimba.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga akizungumza kwenye moja ya vikao vilivyofanyika katika ziara
hiyo.
Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti (katikati) akizungumza jambo kwenye moja ya vikao katika ziara hiyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni