Na. MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya.
·
Amepongeza jitihada
zinazofanywa kulinda miundombinu ya Mahakama mpya za mwanzo.
·
Amepongeza Serikali za
Kata na Vijiji kwa ushirikiano wao katika kuboresha miundombinu ya Mahakama kwa
kusaidia ukarabati na hata kutoa Majengo yao kwa matumizi ya Mahakama.
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu Masijala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Charles Tiganga
amehitimisha ziara ya siku kumi za ukaguzi ulioanza mwanzoni mwa mwezi Juni 2026
kwa kutembelea Mahakama za Wilaya na Mahakama za Mwanzo Mbarali, Chunya, Kyela
na Rungwe zilizopo Masjala Ndogo ya Mbeya.
Lengo
la ukaguzi huo ni kukumbushana juu ya majukumu ya kila siku, kubaini, mapungufu
na changamoto na kuona mapendekezo ya njia sahihi za kukabiliana na changamoto
hizo.
Katika
vikao mbalimbali vilivyofanyika wakati wa ziara hiyo Mhe. Tiganga aliwasisitiza
watumishi kuongeza kasi katika usikilizwaji wa mashauri, kudumisha nidhamu kwa
kuzingatia maadili ya utumishi wa umma na kudumisha ushirikiano kazini.
“Ninawapongeza
kwa kuendelea kudumisha nidhamu, tuendelee kuchapa kazi, tutunze maadili yetu
na ninawapongeza kwa kazi nzuri mnazozifanya na ninawatakieni kila la heri
katika utekelezaji wa majukumu yenu,” alisema Mhe. Tiganga.
Aidha,
Mhe. Tiganga alizipongeza Serikali za Kata na vijiji na wananchi wa maeneo hayo
kwa ushirikiano wao mzuri kwa kuisaidia Mahakama kutekeleza majukumu yake ya
kutoa haki kwa wakati ikiwa ni pamoja na kusaidia katika harakati za ujenzi wa Mahakama
ya Mwanzo Makongorosi iliyopo wilaya ya Chunya na kupatiwa Jengo kwa ajili ya
matumizi ya Mahakama ya Mwanzo Ilongo wilayani Mbarali.
Katika
ziara hiyo Mhe. Tiganga aliongozana na viongozi mbalimbali wa Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya ambao ni Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya
Mbeya Mhe. Aziza Temu, Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Judith
Lyimo, Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Mavis Miti, Hakimu Mkazi
Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Mhe. Zawad Laizer.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga (Katikati) akiwa kwenye picha ya Pamoja na watumishi wa
mahakama ya Wilaya Rungwe
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga (Katikati) akiwa kwenye picha ya Pamoja na watumishi wa Mahakama
ya Wilaya Chunya.
Sehemu ya watumishi wakimsikiliza Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga (hayupo pichani) akiongoza kikao katika ziara hiyo ya ukaguzi.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga (wa tatu kulia) akiwa kwenye picha ya Pamoja na watumishi wa mahakama
ya mwanzo Chimala –Mbarali
Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Judith Lyimo na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Mhe.
Zawadi Laizer, wakipanda mti wa matunda kwa Pamoja katika viunga vya Mahakama
ya Mwanzo Madibira- Mbarali.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga (watatu kulia) akiwa kwenye picha ya Pamoja na watumishi wa
mahakama ya mwanzo Madibira –Mbarali
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga akipanda mti wa matunda katika viunga vya Mahakama ya Mwanzo
Madibira- Mbarali.
Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi.
Mavis Miti akipanda mti wa matunda katika viunga vya Mahakama ya Mwanzo Ndobo
Kyela.
Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Judith Lyimo (aliyesimama) akizungumza jambo kwenye moja ya vikao katika ziara
hiyo.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga akiongoza kikao katika ziara hiyo ya ukaguzi.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga akisaini kitabu cha wageni na baadae akiongoza kikao katika ziara hiyo ya ukaguzi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni