Jumapili, 28 Juni 2026

JAJI MFAWIDHI DODOMA ATETA NA WATUMISHI

  • Asisitiza uadilifu, weledi, uwajibikaji

Na ARAPHA RUSHEKE, Mahakama Kuu Dodoma.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga, ameanza rasmi majukumu yake kwa kukutana na Watumishi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) mara baada ya kuripoti katika kituo hicho.

Katika ziara hiyo aliyoifanya tarehe 22 Juni, 2026, Mhe. Tiganga alitembelea kila ofisi ya mtumishi ili kujionea mazingira ya kazi na kufahamu kwa karibu shughuli zinazotekelezwa na watumishi.

Baadaye, Mhe. Tiganga alifanya kikao na wawakilishi wa watumishi pamoja na wakuu wa vitengo mbalimbali vya Mahakama katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Dodoma.

Katika kikao hicho, alieleza mikakati mbalimbali ya kuimarisha utendaji kazi, ushirikiano na utatuzi wa changamoto zinazoweza kujitokeza katika mazingira ya kazi.

Aidha, Jaji Mfawidhi alisikiliza maoni, ushauri na hoja mbalimbali kutoka kwa watumishi, akisisitiza umuhimu wa mawasiliano ya wazi, uwajibikaji na mshikamano ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za haki kwa wananchi.

Akihitimisha kikao hicho, aliwahimiza watumishi kuendelea kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na kujituma, huku akiahidi kushirikiana nao katika kutafuta suluhisho la changamoto mbalimbali kwa lengo la kuimarisha utendaji wa Mahakama na huduma kwa umma.


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga (aliyekaa katikati) akisema neno wakati wa kikao chake na watumishi waliopo IJC Dodoma, kushoto kwake ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Upendo Ngitiri na kulia kwake ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Dodoma, Bw.Bedson Mariba.

 

Sehemu ya watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma waliohudhuria kikao hicho.


 

Sehemu ya watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma waliohudhuria kikao hicho.


 

Sehemu ya watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma waliohudhuria kikao hicho.


 

Sehemu ya watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma waliohudhuria kikao hicho.


 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni