Jumapili, 21 Juni 2026

JAJI MFAWIDHI MPYA MUSOMA AKABIDHIWA OFISI

Na KANDANA LUCAS-Mahakama Kuu, Musoma

Makabidhiano ya Ofisi ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Musoma, yamefanyika hivi karibuni, kufuatia uhamisho wa mtangulizi wake, Mhe. Fahamu Mtulya kwenda Mahakama Kuu Mbeya.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mhe. Mtulya aliwashukuru Watumishi wa Mahakama Musoma kwa ushirikiano waliompatia katika kipindi cha utumishi wake.  Alisema mafanikio yaliyopatikana yametokana na ushirikiano mzuri kati ya Viongozi na Watumishi, kujituma na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu yao.

Aidha, Mhe. Mtulya aliwaasa Watumishi kuendeleza kudumisha mshikamano na kumpatia ushirikiano Jaji Mfawidhi mpya, Mhe. Edwin Kakolaki, ili kuhakikisha huduma za kimahakama zinaendelea kutolewa kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Mhe. Kakolaki aliahidi kuendeleza mazuri yaliyoanzishwa na mtangulizi wake pamoja na kushirikiana na Watumishi wote katika shughuli za utoaji haki kwa Wananchi.

Vilevile Mhe, Jaji Mfawidhi mpya aliwahimiza Viongozi wote na Watumishi kuendelea kufanya kazi kwa uadilifu, weledi na kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.

Makabidhiano hayo yalihusisha taarifa za utendaji kazi, hali ya mashauri, vifaa vya kazi pamoja na mikakati mbalimbali inayotekelezwa na Mahakama Musoma.

 

Aliyekuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Musoma, Mhe. Fahamu Mtulya Pamoja na Jaji Mfawidhi mpya, Mhe. Edwini Kakolaki, wakipeana taarifa ya makabidhiano ya ofisi. Waliosimama nyuma ni Majaji wa Mahakama Kuu, Naibu Wasajili na Mtendaji wa Mahakama Musoma.

Majaji Wafawidhi wakisaini hati ya makabidhiano ya Ofisi ambapo upande wa kushoto ni Mhe. Fahamu Mtulya, kulia ni Mhe. Edwin Kalokola. Waliosimama kutoka kulia ni Majaji wa Mahakama Kuu Musoma, Mhe. Marlin Komba na Mhe. Kamazima Idd na Naibu Msajili, Mhe. Omari Kingwele, ambao wanashuhudia utiaji wa saini katika hati ya makabidhiano.


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Musoma, Mhe. Edwin Kakolaki, akisalimiana na Watumishi wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma baada ya kuwasili kushiriki makabidhiano ya ofisi.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Songea.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni