Na DHILLON UISSO-Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi, Dar es Salaam
Watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania,
Divisheni ya Ardhi, hivi karibuni walipatiwa mafunzo ili kuwakumbusha kuhusu
mambo mbalimbali, ikiwemo maadili ya utumishi wa umma.
Mafunzo
hayo ya siku mbili yaliyoanza tarehe 18 Juni, 2026, yalijikita pia kuwakumbusha
Watumishi hao kuhusu uwekezaj, afya ya kansa ya mlango wa kizazi, uelewa wa
mifuko ya jamii na bima ya afya.
Akifungua mafunzo hayo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Divisheni ya Ardhi, Mhe. Elinaza
Luvanda, aliwashukuru walioandaa mafunzo
hayo na kusema mafunzo hayo ni muhimu kwa Watumishi.
Mhe.
Luvanda alisema kuwa fursa hiyo siyo tu kufundishana, bali pia ni jambo la
kukumbushana kwakuwa mambo hayo yana zungumzwa mara kwa mara. Pia alizishukuru Taasisi
zilizofadhili na kutoa mada katika
mafunzo hayo.
Maada ya
maadili ilwasilishwa na Jaji wa Mahakama Kuu, Divisheni ya Ardhi, Mhe. Dkt. Eliamani Laltaika, ambapo alisisitiza umuhimu wa maadili kwa Watumishi
wa Umma katika kutenda haki kwa Wadau na Wadaawa wa Mahakama kwa ujumla.
Katika
kuelezea suala la maadili, Watumishi walipata fursa ya kujifunza maana ya
maadili, matawi na umuhimu wa maadili katika utumishi wa umma. Mhe. Dkt.
Laltaika pia alifundisha mambo muhimu ya kuzingatia ili kutokuvunja maadili kwa
Watumishi wa umma kwa maongezi, vitendo, mavazi na utendaji wa kazi kwa ujumla.
Katika
mafunzo hayo, Watumishi pia walipata mafunzo juu ya umuhimu wa kupima afya zao
mara kwa mara, hususani kupima saratani ya mlango wa kizazi kwa wanawake.
Mafunzo
hayo pia yalihusisha maafisa kutoka UTT, PSSSF na NHIF, ambao kwa ujumla wao
walielezea muhimu wa uwekezaji, fao la uzeeni na bima ya afya kwa Watumishi.
Mafunzo hayo yalihitimishwa na Kaimu Jaji Mfawidhi,
Mahakama Kuu, Divisheni ya Ardhi, Mhe. Mohamed Gwae, ambaye aliwashukuru
waandaaji kwa kufanikisha mafunzo hayo.
Alieleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwakuwa yanajenga mahusiano bora katika kazi. Mhe. Gwae aliwataka Watumishi kuzingatia maadili ya utumishi wa umma kama walivyo fundishwa.
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi, Mhe. Elinaza Luvanda, (wa pili kushoto), wengine ni Majaji wa Mahakama Kuu, Mhe. Dkt. Thedora Mwenegoha, Mhe. Dkt. Eliamani Laltaika na Mhe. Monica Otaru.
Jaji wa Mahakama
Kuu Divisheni ya Ardhi, Mhe. Dkt. Eliamani Laltaika, akiwasilisha mada kuhusu
maadili kwa utumishi wa umma.
Picha za pamoja
baada ya kuhitimishwa mafunzo hayo. Katikati waliokaa ni Kaimu Jaji Mfawidhi,
Mahakama Kuu, Divisheni ya Ardhi, Mhe. Mohamed Gwae.







Hakuna maoni:
Chapisha Maoni