Jumatatu, 29 Juni 2026

JAJI MFAWIDHI MTWARA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MAHAKAMA

Na MWANDISHI WETU-Mahakama, Mtwara

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule, hivi karibuni amefanya ziara ya ukaguzi wa Mahakama za Mkoa wa Mtwara ili kujionea utendaji kazi ili kuhakikisha huduma ya utoaji haki inaendelea kufanya vyema.

Miongoni mwa Mahakama zilizokaguliwa ni Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mahakama za Wilaya Tandahimba, Newala, Nanyumbu, Masasi na Mahakama za Mwanzo Litehu, Mnyambe, Nakopi, Chiungutwa.

Ziara hiyo pia ilijumuisha mazungumzo ya pamoja na Watumishi wa Mahakama alizopita kwa ajili ya ukaguzi. Aliweza kupata taarifa za utendaji kazi, mafanikio, changamoto, mapato na matumizi.

Mhe. Mteule aliwapongeza Mahakimu na Watumishi wa Mahakama kwa utendaji bora na mzuri, hasa kumaliza mashauri kwa wakati, kutokuwa na mlundikano.

Katika ukaguzi huo pia, Jaji Mfawidhi aliwapongeza Watumishi wa Mahakama katika matumizi wa mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ambayo inawezesha kufuatilia na kusikiliza mashauri kwa njia ya mtandao. Aliwasisitiza kuendelea kuwaelewesha Wananchi kwenye matumizi ya mifumo hiyo ili kupunguza gharama za kila mara.

Katika ziara hiyo, Jaji Mfawidhi aliambatana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Mtwara, Mhe. Seraphine Nsana, Mtendaji wa Mahakama Mtwara, Bw. Yusuph Msawanga na Msaidizi wa Sheria wa Jaji Mfawidhi, Mhe. Stella Shindika.

Jaji Mfawidhi pia alitembelea na kukagua Mahakama ya Wilaya Masasi iliyopo katika ujenzi na kusisitiza ufanyike kwa kuzingatia ubora na kwenda kwa wakati.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule akisalimiana na Mahakimu na Watumishi katika Mahakama ya Wilaya Newala.

 

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule, akipanda mti wa ukumbusho katika Mahakama ya Wilaya Newala.

 

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule akiwa katika ukaguzi wa eneo la Mahakama ya Mwanzo Mnyambe iliyopo Wilaya ya Newala.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule akisalimiana na Mahakimu, Watumishi na Wadau baada ya kuwasili katika Mahakama ya Wilaya Nanyumbu.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule (kushoto mbele) akiwa kwenye ukaguzi wa eneo la Mahakama ya Mwanzo Litehu.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule (kulia) akiwa kwenye ukaguzi wa jengo jipya la Mahakama ya Wilaya Masasi lililopo kwenye ujenzi unaondelea.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule (katikati) akiwasikiliza Watumishi katika kikao kilichifanyika Mahakama ya Wilaya Tandahimba.

 

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule (katikati) akipata picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Chiungutwa.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Litehu.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Mwanzo Nakopi.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Nanyumbu.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Newala.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Tandahimba.

 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Masasi.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Singida.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni