Na. MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania, Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya,
ameongoza kikao cha usimamizi wa mwenendo wa mashauri ya jinai (Case Flow
Management) kilichofanyika tarehe 25 Juni 2026 katika ukumbi wa mikutano wa
Mahakama Kuu Mbeya kwa lengo la kujadili mwenendo wa mashauri ya jinai na hali
ya upatikanaji wa haki jinai.
Kikao
hicho kilihudhuriwa na Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Mussa
Pomo, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya, Mhe. Judith Lyimo,
Naibu Msajili wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Mhe. Zawadi Laizer, Mahakimu
pamoja na wadau mbalimbali wa haki jinai.
Miongoni
mwa masuala yaliyojadiliwa ni mustakabali wa mashauri ya jinai ya mlundikano na
yanayotarajiwa kuingia kwenye mstari wa mlundikano ifikapo Disemba, 2026,
ambapo mikakati iliwekwa ili kuhakikisha kuwa mashauri hayo yanamalizika hadi
ifikapo Novemba 2026.
Aidha,
kikao hicho pia kilipitia kwa pamoja utekelezaji wa maazimio ya kikao kilichopita,
ikiwemo uteketezaji wa vielelezo vya madawa ya kulevya ambao ulitekelezwa tangu
mwezi Mei, 2026 ikiwa ni katika mikakati ya kupunguza mlundikano wa vielelezo mahakamani.
Vilevile,
Mhe. Mtulya aliielekeza Ofisi ya Mwendesha Mashtaka (NPS) kupitia majalada ya
mashauri 26 yanayotarajiwa kuwa ya mlundikano ifikapo mwezi Disemba, 2026 ili
kuandaa vikao maalum vitakavyosaidia kuharakisha usikilizwaji wa mashauri hayo.
Naye,
Naibu Msajili Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Mhe. Zawadi Laizer alisisitiza
ushirikiano wa taasisi zote za haki jinai katika kutekeleza majukumu yao kwa
wakati.
Kwa
upande wake, Naibu Msajili Mahakama Kuu masjala ndogo ya Mbeya Mhe. Judith Lyimo
aliiomba taasisi ya Magereza kuwasaidia wafungwa kusajili mashauri yao kwa
wakati.
Nao,
Magereza walipendekeza wafungwa walio tayari kukiri makosa yao wasikilizwe
mapema ili kurahisisha mwenendo wa mashauri, huku Mawakili wa Serikali kutoka
Ofisi ya Mwendesha Mashitaka (NPS) wakiahidi kutekeleza maelekezo yote
yaliyotolewa katika kikao hicho.
Kikao
hicho ni sehemu ya jitihada za wadau wa haki jinai Masjala Ndogo ya Mbeya za
kuimarisha usimamizi wa mashauri na kuhakikisha wananchi wanapata haki kwa
wakati mapema ipasavyo.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya
Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akizungumza katika kikao hicho, kulia ni Naibu
Msajili Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Mhe. Zawadi Laizer na kushoto ni Jaji wa
Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo.
Sehemu ya washiriki wa kikao hicho wakimfuatilia kwa
makini Mwenyekiti wa kikao hicho Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya
Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya Mhe. Fahamu Mtulya (hayupo pichani).
Sehemu ya washiriki wa kikao hicho wakimfuatilia kwa
makini Mwenyekiti wa kikao hicho Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya
Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya Mhe. Fahamu Mtulya (hayupo pichani).
Naibu Msajili Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Mhe.
Zawadi Laizer akiwasilisha taarifa katika kikao hicho, kushoto ni
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni