Na. ALLY RAMADHANI – Mahakama, Katavi
Ofisi
ya Taifa ya Mashtaka (NPS) Kanda ya Magharibi inayojumuisha mikoa ya Katavi,
Kigoma na Tabora tarehe 19 Juni, 2026 waliandaa bonanza la kimichezo lililojumuisha
michezo mbalimbali kama vile mpira wa miguu, netiboli, kukimbiza kuku, kukimbia
na gunia, kuvuta Kamba na kukuna nazi.
Kwa
upande wa Mahakama kama mgeni mwalikwa kwenye bonanza hilo, waliondoka na
medali za ushindi kwenye michezo ya kukimbiza kuku kwa mtumishi Bi. Jihadat
Ntimba, mchezo wa kukuna nazi kwa wanaume alishinda Mhe. Mohamed Shabani, kukimbia
na gunia kwa wanaume Bw. Ally Rajab, mchezo wa kuvuta kamba ushindi ukienda kwa
NPS, huku mechi ya mpira wa miguu ikiisha kwa suluhu ya bila kufungana baina ya
NPS na Polisi Katavi.
Kupitia
bonanza hilo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo Katavi,
Mhe Godfrey Ntemi Isaya amempongeza Mkuu wa Mashtaka Katavi Bw. Theophil
Mutakyawa Daniel kwa kuwa mwenyeji wa bonanza hilo lililoikutanisha mikoa hiyo
na kupata fursa ya kujumuika pamoja na kubadilishana uzoefu.
“Leo
tumepata nafasi ya kufanya mazoezi kwa pamoja ambayo yanatusaidia kuimarisha
afya zetu, vilevile mabonanza kama haya yanasadia kuimarisha umoja, upendo, na
mshikamano miongoni mwetu na kufanya kazi kama timu…”
…
Leo tumepata nafasi ya kukutana kwa pamoja kati yetu sisi Mahakama, NPS,
Polisi, TAKUKURU, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Katavi na jamii yetu ya wananchi wa
mkoa wetu wa Katavi, ninachotaka kukimaanisha hapa ni kwamba utendaji kazi wetu
mzuri kwa jamii yetu utasaidia kuimarisha amani na utulivu tulionao Katavi,” alisema
Mhe. Isaya.
Vilevile,
kupitia bonanza hilo Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Bw. Albert Msovela kwa niaba
ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi ameipongeza Mahakama ya Tanzania kwa kuanzisha huduma
za Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Katavi kwa kuwa hapo kabla wananchi wa Katavi
walikua wakipata changamoto nyingi wanapofuata huduma hizo Mkoani Rukwa
(Sumbawanga).
Aidha,
ameipongeza Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa mikoa yote mitatu Kigoma, Tabora na
Katavi kwa kitu walichokifanya kwani kinaongeza umoja, mshikamano na upendo
miongoni mwao.
Mkuu
wa Mashtaka Mkoa wa Katavi, Bw. Theophil Mutakyawa Daniel ametoa shukrani zake
kwa wageni waalikwa wote huku akiishukuru sana Mahakama Kuu ya Tanzania kwa kusogeza
karibu zaidi huduma za Mahakama Kuu mkoani Katavi kwani imesaidia kutatua
changamoto nyingi zilizokua zinawakumba hasa wananchi mkoani hapo.
Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa mikoa ya Tabora, Kigoma na Katavi wakiwa katika picha ya Pamoja na baadhi ya viongozi wa Taasisi mbalimbali mkoani Katavi walioketi kwenye viti mbele ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Katavi Mhe. Jaji Godfrey Ntemi Isaya wa pili kushoto, Katibu tawala wa Mkoa Bw. Albert Msovela (aliyekaa katikati mwenye kofia), wa kwanza kulia ni RPO Bw. Theophil Mutakyawa Daniel Mkuu wa Mashtaka Katavi, wa pili kulia ni RPO Bi. Chema, Mkuu wa Mashtaka Tabora na wa kwanza Kushoto ni RPO Bw. Magumbo Mkuu wa Mashtaka Kigoma.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala
Ndogo ya Katavi Mhe. Godfrey Ntemi Isaya, akiongea na wananchi kwenye bonanza
lililoandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa Mikoa ya Tabora, Kigoma na
Katavi lililofanyika viunga vya Shule ya Sekondari Rungwa iliyopo Mjini Mpanda
Katavi.
Mshindi wa Mchezo wa Kukuna nazi kwa upande wa wanaume Mhe. Mohamed Masoud Shabani Mtumishi wa Mahakama Kuu Katavi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Bw. Albert
Msovela kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi, akitoa shukrani zake kwa washiriki
wote wakati wa bonanza lililoandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa Mikoa ya
Tabora, Kigoma na Katavi lililofanyika viunga vya Shule ya Sekondari Rungwa
iliyopo Mjini Mpanda Katavi.
Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala
Ndogo ya Katavi Mhe. Silivia Lushasi, akifuatilia kwa ukaribu wakati wa bonanza
lililoandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa Mikoa ya Tabora, Kigoma na
Katavi lililofanyika viunga vya Shule ya Sekondari Rungwa iliyopo Mjini Mpanda
Katavi.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha-Mahakama)

.jpeg)


.jpeg)

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni