Alhamisi, 18 Juni 2026

WATUMISHI DODOMA WAMPONGEZA NAIBU MSAJILI MPANGULE

Na ARAPHA RUSHEKE, Mahakama Kuu Dodoma.

Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dodoma, Mhe Biswalo Mganga, amewaongoza Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma katika hafla fupi ya kumpongeza Mhe. Zabibu Mpangule, mara baada ya kuteuliwa na kuapishwa kuwa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Dodoma.

Hafla hiyo imefanyika tarehe 17 Juni 2026 katika ukumbi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Dodoma.

Akizungumza kwa niaba ya watumishi, Mhe. Mganga amempongeza Mhe. Mpangule kwa kuaminiwa na kupewa nafasi hiyo muhimu, akieleza kuwa uteuzi wake ni matokeo ya utendaji kazi uliotukuka, uadilifu na kujituma katika kutekeleza majukumu yake.

Kabla ya uteuzi huo, Mhe. Mpangule alikuwa akihudumu kama Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma ambapo alitoa mchango mkubwa katika utoaji wa huduma za haki kwa Wananchi.

Kwa upande wake, Mhe. Mpanguke aliwashukuru Watumishi kwa pongezi zao na kuhahidi kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa weledi, uadilifu na kujituma kwa manufaa ya Mahakama na Wananchi kwa ujumla.

Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma pamoja na Wilaya zake walimtakiwa kila la kheri katika majukumu yake mapya.

Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Biswalo Mganga (wa kwanza kushoto) akimkabidhi zawadi Naibu Msajili, Mhe. Zabibu Mpangule, katika hafla ya kumpongeza.

Watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja na kumpatia dhawadi  Naibu Msajili mteule (wa nne kutoka kushoto).

 

Naibu Msajili, Mhe. Zabibu Mpangule akikata keki ambayo ameandaliwa katika hafla ya kumpongeza.

Watumishi wa Mahakama Dodoma waliohudhuria hafla hiyo wakiwa katika picha ya pamoja wakifanya ibada kabla ya kuanza hafla hiyo.

Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja mara baada kumpokea Naibu Msajili, Mhe. Zabibu Mpangule, mara baada ya kuwasili kutokea kula kiapo katika Ofisi za Tume ya utumishi wa Mahakama.

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni