Jumapili, 28 Juni 2026

ZIARA YA UKAGUZI WA GEREZA KUU LILUNGU MTWARA

Na MWANDISHI WETU-Mahakama, Mtwara

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule, hivi karibuni amefanya ziara ya ukaguzi na kutembelea Gereza Kuu la Lilungu katika Mkoa wa Mtwara, ili kujionea utendaji kazi wa Gereza hilo.

Ziara hiyo ilijumuisha pia mazungumzo ya pamoja na Askari Magereza na kufanya ukaguzi wa mazingira na kupata taarifa za utendaji kazi, mafanikio na changamoto.

Aidha, Jaji Mfawidhi pia alizungumza na kusikiliza changamoto za Wafungwa, mawazo na maoni kutoka kwa Watumishi kutoka kwa Wadau.

Mhe. Mteule aliahidi kujibu changamoto ambazo zilizokuwa katika meza yake kwa upande wa Mahakama, na kuwaomba kila mmoja kuweza kushiriki utendaji kazi bora katika maeneo yanayohusu Magereza.

Aliwasisitiza matumizi ya TEHAMA kwa wale ambao mashauri yao bado kwenye kusikilizwa na kuhakikisha kunakuwa na uwezekano wa kupunguza gharama za kila mara.

Katika ziara hiyo, Jaji Mfawidhi aliambatana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Mtwara, Mhe. Seraphine Nsana, Mtendaji wa Mahakama Mtwara, Bw. Yusuph Msawanga na Msaidizi wa Sheria wa Jaji Mfawidhi, Mhe. Stella Shindika.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule, akipokelewa na Askari Magereza wakati wa ziara yake.

 

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule, akipata picha ya pamoja na Askari Magereza pamoja na Wadau mbalimbali.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Mtwara, Mhe. Katarina Mteule, (katikati) akipata picha ya pamoja baada ya kumaliza ziara ya ukaguzi.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Singida.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni