Na. MWANDISHI WETU - Mahakama, Dodoma
Jaji
Mkuu wa Tanzania Mhe. George Masaju leo tarehe 8 Julai, 2026 ameungana na
familia, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na watumishi wa Mahakama kutoa heshima
za mwisho kwa aliyekuwa Mtumishi wa Mahakama ya Wilaya Kaliua, Hakimu Mkazi
Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kaliua, Mhe. Anna Elia Chilongola aliyefariki
dunia tarehe 3 Julai, 2026.
Ibada
na shughuli za mazishi zimefanyika katika Mtaa wa Chang'ombe Dispensari, jijini
Dodoma nyumbani kwa marehemu, ambapo viongozi mbalimbali wa Mahakama kutoka
Makao Makuu ya Mahakama, Masjala Ndogo za Dodoma na Tabora wakiwemo Majaji wa
Rufani na Mahakama Kuu, Wasajili, Naibu Wasajili, Mahakimu, watumishi wa Mahakama
pamoja na viongozi kutoka Taasisi mbalimbali zinazofanya kazi na Mahakama
katika ngazi mbalimbali walihudhuria kushiriki katika kumuaga marehemu Anna.
Jaji
Mkuu alifika katika eneo la mazishi na kushiriki kutoa heshima za mwisho kwa
marehemu pamoja na kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na watumishi
wa Mahakama waliofiwa na mwenzao, kabla ya kuondoka kuendelea na majukumu
mengine ya kitaifa yaliyokuwa amejipangia.
Kwa
upande wake, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Dodoma Joachim
Tiganga akitoa salaam za pole kwa niaba ya Mahakama ya Tanzania amesema kuwa,
marehemu alikuwa muadilifu, mwenye weledi, mchapa kazi hondari na hata alipokea salamu
kutoka kwa Jaji Kiongozi akielezea umahiri wake katika kuchapa kazi enzi za
uhai wake.
“Ni
kweli usiopingika kwamba Mahakama ya Tanzania imempoteza mlezi wa Mahakimu
wachanga waongia kazini kwani kwa sehemu kubwa Mahakama ilimtumia pia kama mlezi wa
watumishi wengine katika kazi za kila siku za utoaji haki,” amesema Jaji
Tiganga.
Mahakama
ya Tanzania inatoa pole kwa familia ya Marehemu, Ndugu, Jamaa, Marafiki na wafanyakazi
wote wa Mahakama ili azidi kuombewa na kupata pumziko la milele.
Wakizungumza
wakati wa shughuli hizo, viongozi mbalimbali walimkumbuka Mhe. Anna Elia
Chilongola kuwa mtumishi aliyekuwa mwadilifu, mchapakazi na mwenye kujituma
katika utekelezaji wa majukumu yake, pia alikuwa Mchamungu huku wakieleza kuwa
mchango wake katika utumishi wa Mahakama utaendelea kukumbukwa.
Mahakama ya Tanzania inaendelea kutoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na watumishi wote walioguswa na msiba huu, ikiomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
Jeneza lililobeba mwili wa Marehemu aliyekuwa Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kaliua, Mhe. Anna Elia Chilongola aliyefariki dunia tarehe 3 Julai, 2026.











Hakuna maoni:
Chapisha Maoni