Jumamosi, 25 Julai 2026

JAJI MKUU MASAJU ASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA TANZANIA

Na MARY GWERA, Mahakama - Dodoma

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju leo tarehe 25 Julai, 2026 ameungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (JWTZ) Jenerali Jacob John Mkunda, Viongozi wa Serikali na Watanzania wote kwa ujumla kuadhimisha Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa nchini.

Hafla ya  Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa nchini imefanyika katika Viwanja vya Mashujaa vilivyopo katika Mji wa Serikali-Mtumba jijini Dodoma huku ikitawaliwa na ratiba mbalimbali ikiwemo utoaji wa dua na sala.

Katika maadhimisho hayo, Viongozi mbalimbali pia walishiriki kutoa heshima kwa kuweka vifaa na alama za jadi kwenye Mnara wa Mashujaa wakiongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye aliweka Mkuki na Ngao kwenye Mnara wa Kumbukumbu ya Mashujaa ikiwa ni ishara ya kuwaenzi, kuwakumbuka na kuthamini mchango wa mashujaa waliopigania uhuru, amani na maendeleo ya Taifa.

Kadhalika Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda aliweka Sime; Balozi wa Burundi nchini Tanzania, Mhe. Leontine Nzeyimana aliweka shada la maua kwa niaba ya Mabalozi, Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe. Alimwoni Chaula aliweka Upinde na Mshale huku Brigedia Jenerali (Mstaafu), Wilfred Paul Mwakalambile Kabunda akiweka Shoka.

Mbali na Jaji Mkuu, Viongozi wengine waliohudhuria katika Sherehe hizo ni pamoja na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Emmanuel John Nchimbi,  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule na wengine.

Aidha kwa upande wa Mahakama, sherehe hizo zimehudhuriwa pia na Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Sam Rumanyika, Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Antony Jingu, Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Chiganga Tengwa na baadhi ya Viongozi wengine.

Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa Tanzania huadhimishwa tarehe 25 Julai kila mwaka lengo likiwa ni kuwakumbuka na kuwaenzi Mashujaa wote waliopoteza maisha yao wakitetea, kupigania na kulinda uhuru, amani, umoja na maslahi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Maadhimisho hayo yanaendelea kuwa chachu ya kuhamasisha uzalendo, mshikamano na uwajibikaji kwa vizazi vya sasa na vijavyo katika kulijenga Taifa la Tanzania.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (katikati) akiwa katika sherehe za Siku ya Kumbukumbu ya  Mashujaa Tanzania leo tarehe 25 Julai, 2026 katika Viwanja vya Mashujaa vilivyopo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma. Wa pili kushoto ni  Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (JWTZ) Jenerali Jacob John Mkunda, anayefuata ni Balozi wa Burundi nchini Tanzania, Mhe. Leontine Nzeyimana, anayefuata ni Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe. Alimwoni Chaula na wa kwanza kulia ni Brigedia Jenerali (Mstaafu), Wilfred Paul Mwakalambile Kabunda.
Matukio katika picha Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa Nchini leo tarehe 25 Julai, 2026 
katika Viwanja vya Mashujaa vilivyopo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju akiingia katika Viwanja vya Mashujaa vilivyopo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma leo tarehe 25 Julai, 2026. 


Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Sam Rumanyika (wa pili kushoto) akifuatiwa na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Antony Jingu, akifuatiwa na Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Chiganga Tengwa, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanania na Katibu wa Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Venance Mlingi na Katibu Msaidizi wa Jaji Mkuu, Mhe. Wilberforce Luhwago wakiwa katika Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa Tanzania leo tarehe 25 Julai, 2026 katika Viwanja vya Mashujaa vilivyopo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma. 

Vikosi mbalimbali vya Gwaride maalum vilivyoandaliwa kwa ajili ya Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa Tanzania.

Baadhi ya Maofisa kutoka Mahakama ya Tanzania waliohudhuria katika sherehe za Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa Tanzania.

Picha mbalimbali za matukio ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa nchini leo tarehe 25 Julai, 2026 katika Viwanja vya Mashujaa vilivyopo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma. 

Burudani ikiendelea.

Mnara wa Mashujaa.

Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju akiondoka  katika Viwanja vya Mashujaa-Mtumba jijini Dodoma mara baada ya kukamilika kwa sherehe hizo.

                         (Picha na MARY GWERA, Mahakama)



 


 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni