- Wamkaribisha pia Jaji Otaru
Na DHILLON
UISSO – Mahakama Ardhi Dar es Salaam
Watumishi
wa Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi, tarehe 17 Julai, 2026 walishiriki katika
hafla ya kumuaga aliyekuwa Jaji Nehemia Mandia, Jaji, aliyehamishiwa Mahakama Kuu
Divisheni ya Kazi.
Katika hafla hiyo, Waumishi pia walimkaribisha Jaji wa Mahakama Kuu, Mhe. Monica Otaru, ambaye amehamia Divisheni ya Ardhi, maarufu udongoni.
Hafla
hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi na kuhudhuriwa
na Kaimu Jaji Mfawidhi, Mhe. Arafa Msafiri na baadhi ya Majaji na Naibu Wasajili,
Mtendaji wa Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi, pamoja na Watumishi.
Akizungumza
wakati wa hafla hiyo, Mhe. Msafiri alimpongeza Mhe. Mandi kwa ushirikiano,
upendo na mchango mkubwa kipindi chote alichohudumu katika Divisheni ya Ardhi.
“Tunakupongeza
sana Mhe. Mandia kwa uchapakazi, upendo na ushirikiano wako na ukawe balozi
wetu huko. Wewe bado ni mwana udongoni,” alisema.
Kaimu
Jaji Mfawidhi alitumia fursa hiyo kumkaribisha Mhe. Otaru kwa kujiunga na timu
ya Divisheni ya Ardhi yenye upendo na ushirikiano mkubwa.
“Najua wewe
ni mchapakazi na mwenye upendo mkubwa, karibu sana kwenye familia ya udongoni. Tutakupa
ushirikiano na “team work,” Mhe. Msafiri alisema.
Kwa
upande wake, Mhe. Mandia alitoa shukrani kwa Majaji, Viongozi wengine na watumishi
wote aliobahatika kufanya nao kazi kwa kipindi chote. Alisema ushirikiano,
upendo na mshikamano alioupata kutoka kwao ulichangia mafanikio yake katika
kazi za kila siku.
Aliwaasa
kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, bidii na uaminifu, akisisitiza
kuwa mafanikio katika utumishi yanatokana na kuipenda kazi na kutimiza wajibu
kwa moyo wa kujituma.
Naye Mhe. Otaru alitoa neno la kushukuru kwa kukaribishwa na kuanza kushughulikia majalada kwa kasi na ushirikiano kutoka kwa Majaji, Viongozi na Watumishi kwa ujumla na kufanya kazi yake kuwa rahisi.
Majaji wa Mahakama Kuu, Mhe. Nehemia Mandi na Mhe. Monica Otaru, wakikata keki.
Kaimu Jaji Mfawidhi, Mhe. Arafa Msafiri, akimkabidhi Mhe. Mandia zawadi.
Majaji wa Mahakama Kuu wakifurahia jambo wakati wa hafla hiyo.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni