Na. MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya
Watumishi
wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya wamehitimisha mafunzo ya siku mbili ya
namna bora ya kuandaa kumbukumbu za rufaa za mashauri ya jinai, yaliyofanyika
hivi karibuni jijini Mbeya yakilenga kuimarisha ufanisi katika uandaaji wa
nyaraka na kumbukumbu za Mahakama ya Rufani.
Mafunzo
hayo yalifunguliwa na Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya
Mbeya, Mhe. Benard Mpepo, ambaye alisisitiza umuhimu wa watumishi wa kada zote
kuwa na uelewa wa pamoja kuhusu taratibu za uandaaji wa kumbukumbu za rufaa na
kuongeza kuwa, ubora wa uandaaji wa nyaraka za Mahakama ni msingi muhimu wa utoaji
wa haki kwa wakati.
Washiriki
wa mafunzo hayo walitoka kada mbalimbali ikiwemo Mahakimu, wasaidizi wa
kumbukumbu, waandishi waendesha ofisi, wasaidizi wa ofisi na walinzi, hatua
inaonesha dhamira ya Mahakama ya kuwajengea uwezo watumishi wote ili kuboresha
utendaji kazi wa taasisi.
Akitoa
mada katika mafunzo hayo, Hakimu Mkazi wa Mahakama Kuu Mbeya, Mhe. Hassan
Yahaya Mbojellah, aliwaelekeza washiriki kuhusu taratibu na mambo muhimu ya
kuzingatia wakati wa kuandaa kumbukumbu za Mahakama ya Rufani kwa mashauri ya
jinai.
Alifafanua
tofauti za uandaaji wa kumbukumbu kwa mashauri yanayotoka Mahakama za Mwanzo,
Mahakama za Wilaya na Mahakama za Hakimu Mkazi, pamoja na mashauri yenye asili
ya Mahakama Kuu.
Mbali
na mafunzo ya nadharia, washiriki walipata fursa ya kujifunza kwa vitendo
kupitia kazi za makundi, ambapo waliandaa kumbukumbu za rufaa na vitabu
mbalimbali vya Mahakama ya Rufani kwa kutumia mifano halisi. Mbinu hiyo
iliwawezesha kuongeza uelewa na umahiri katika kuandaa nyaraka kwa kuzingatia
viwango vinavyotakiwa.
Kwa
upande wao, washiriki walieleza kuridhishwa na mafunzo hayo na kuomba yawe
endelevu, wakisema yatawasaidia kuongeza uelewa kuhusu masuala ya mashauri,
uandaaji na utunzaji wa kumbukumbu za mahakama.
Washiriki
wa mafuzo hayo walisisitiza kuwa, kwa kuwa mashauri ndiyo kiini cha shughuli za
Mahakama, mafunzo ya mara kwa mara yataongeza ubora wa huduma na ufanisi katika
utekelezaji wa majukumu yao.
Mafunzo
hayo ni sehemu ya juhudi za Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya za kuendelea
kuwajengea uwezo watumishi wake, kuboresha usimamizi wa mashauri na kuhakikisha
nyaraka na kumbukumbu za Mahakama ya Rufani zinaandaliwa kwa usahihi kwa
kuzingatia weledi, taratibu na viwango vinavyotakiwa.
Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Benard Mpepo akifungua mafunzo ya siku mbili ya namna bora ya kuandaa kumbukumbu za rufaa za mashauri ya jinai kwa watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeyav (hawapo pichani).
Mtoa
mada katika mafunzo hayo Hakimu Mkazi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Hassan Yahaya Mbojellah (aliyesimama) akitoa madini katika mafunzo hayo.
Mtoa
mada katika mafunzo hayo Hakimu Mkazi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Hassan Yahaya Mbojellah (aliyesimama) akitoa madini katika mafunzo hayo.
Kaimu Mtendaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bw. Alintula Watson Ngalile (aliyesimama) akizungumza katika mafunzo hayo, kulia ni Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Benard Mpepo.
Msaidizi
wa Ofisi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Bi. Editha Exavery Mhiliwa
(aliyesimama) akieleza kwa muhtasari mada zilizofundishwa katika siku ya kwanza
ya mafunzo hayo.
Sehemu
ya Watumishi walioshiriki katika Mafunzo hayo.
Sehemu
ya Watumishi walioshiriki katika Mafunzo hayo.
Sehemu
ya Watumishi walioshiriki katika Mafunzo hayo.
Sehemmu
ya washiriki katika mafunzo hayo wakiwa kwenye makundi wakifanya kwa
vitendo yale waliyojifunza ambapo ilikuwa ni sehemu ya mafunzo hayo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni