Na CHRISTOPHER MSAGATI - Mahakama, Manyara
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi
amemtembelea Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga ofisini kwake
jana tarehe 20 Agosti, 2026 kwa ajili ya kujitambulisha kwa viongozi na wadau wa
Mkoa wa Manyara tangu alipohamia Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Manyara Mwezi
Juni, 2026.
Mhe.
Dkt. Mambi alimshukuru Mhe. Sendiga kwa kumkaribisha ofisini kwake kwa ajili ya
mazungumzo, kufahamiana na kujadiliana juu ya utendaji kazi na ushirikiano
unaopaswa kuwepo baina ya Ofisi hizo.
Aidha,
Mhe. Dkt. Mambi alimuomba Mkuu wa Mkoa huyo aweze kusaidia katika suala la
upatikanaji wa viwanja kila Kata za Mkoa wa Manyara kwa ajili ya ujenzi wa
Mahakama za Mwanzo.
“Kwa
kuwa huduma za Mahakama zinaendelea kukua kila siku, tunaomba utusaidie katika
michakato mzima wa kupata viwanja pamoja na hati za umiliki katika Kata ambazo
hamna huduma za Mahakama ili tuweze kujenga Mahakama hizo na kusogeza huduma karibu
na wananchi,” alisema Mhe. Dkt. Mambi.
Kwa
upande wake, Mhe. Sendiga alimuahidi Mhe. Dkt. Mambi kutekeleza jukumu hilo kwa
kuwasiliana na mamlaka zilizopo chini yake ili viwanja hivyo vipatikane ili
kukidhi adhima ya Mahakama ya kusogeza huduma za haki karibu na wananchi.
“Ninatambua
kuwa Mkoa wetu wa Manyara una changamoto ya uhalifu na hususan mashauri ya
kijinsia, na kwa sababu hiyo ni kweli kila mahali panahitaji kufikiwa na huduma
hizi za Mahakama. Kwa sababu hiyo Mhe Jaji nitajitahidi kuwasiliana na viongozi
wa Mamlaka nyingine ili tufanikiwe katika upatikanaji wa viwanja na hati hizo,”
alisema Mhe. Sendiga.
Katika
hatua nyingine, Mhe. Dkt. Mambi, alikukutana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya
Mkoa kwa ajili ya kujitambulisha na kufanya nao mazungumzo juu ya ushirikiano
wa Taasisi zao katika mnyonyoro wa Utoaji haki. Viongozi hao wa Kamati ya
Ulinzi na Usalama walimkaribisha na kumuahidi ushirikiano wa kutosha katika
kuhakikisha kazi za Mahakama zinakwenda ipasavyo.
Katika
ziara hiyo, Mhe. Dkt. Mambi aliambatana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu,
Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Charles Mnzava na Mtendaji wa Mahakama Kuu,
Masjala Ndogo ya Manyara Bi. Nyanzobe Hemei.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Manyara, Mhe. Dkt. Adam Mambi (wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen
Sendiga (katikati), (wa pili kushoto) ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo
ya Manyara Mhe. Charles Mnzava, (kulia) ni Mtendaji wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo
ya Manyara Bi. Nyanzobe Hemed, na (kushoto) ni Hakimu Mkazi na
Msaidizi wa Sheria Mhe. Kuruthumu Mkundawantu.
Naibu
Msajili wa Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Manyara Mhe Charles Mnzava
(aliyesimama) akichangia jambo wakati wa mazungumzo kati ya Jaji Mfawidhi wa
Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Manyara, Mhe. Dkt. Adam Mambi na Kamati ya Ulinzi
na Usalama ya Mkoa wa Manyara.
Mtendaji
wa Mahakama Kuu, Masjala ndogo ya Manyara Bi. Nyanzobe Hemed (kushoto)
akifuatilia mazungumzo kati ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya
Manyara, Mhe. Dkt. Adam Mambi na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga
walipomtembelea Mkuu huyo wa Mkoa Ofisini kwake na kulia ni Hakimu Mkazi na
Msaidizi wa Sheria Mhe. Kuruthumu Mkundawantu.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga (katikati) akichangia neno mbele ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara, Mhe. Dkt. Adam Mambi (kulia) pamoja na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Charles Mnzava mara baada ya kumtembelea ofsini kwake.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara Mhe. Dkt. Adam Mambi akiwa
anamsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga (hayupo pichani) mara
baada ya kumtembelea ofisini kwake.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Manyara, Mhe. Dkt. Adam Mambi
(aliyekaa kwenye kiti) akiwa katika picha ya pamoja na timu ya viongozi wa
Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Manyara na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa
wa Manyara.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)
.jpg)
.jpg)
%20(1).jpg)
%20(1).jpg)
.jpg)
%20(1).jpg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni