Na ARAPHA RUSHEKE -Mahakama, Dodoma
Jaji
Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, jana tarehe
10 Agosti, 2026, alifanya ziara katika jengo la zamani la Mahakama Kuu Dodoma,
linalotarajiwa kutumika kwa ajili ya Mahakama inayoshughulikia masuala ya
familia.
Akiwa
ameambatana na Viongozi mbalimbali wa Mahakama, Jaji Kiongozi alikagua
miundombinu ya jengo hilo na kujionea maboresho yanayoendelea kufanyika.
Katika
ziara hiyo, Mhe. Dkt. Siyani aitoa maelekezo mbalimbali yanayolenga kusaidia
katika uboreshaji wa miundombinu na
mazingira ya jengo hilo, ili liweze kuwa na mazingira bora kwa ajili ya
utoaji wa huduma za haki kwa wananchi.
Ziara
hiyo ni sehemu ya jitihada za Mahakama katika kuhakikisha miundombinu yake
inaendelea kuboreshwa, sambamba na kuimarisha mazingira ya utoaji wa huduma za
haki.
PICHA CHINI ZINAOONESHA ZIARA HIYO

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, akiendelea na ukaguzi mara baada ya kuwasilia katika jengo la zamani la Mahakama Kuu Dodooma, ambalo linatarajiwa kuwa Mahakama ya Familia Dodoma.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, akiangalia sehemu ya mapokezi ya jengo hilo ambalo linatarajiwa kuwa Mahakama ya Familia Dodoma.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, akisikiliza maelezo ambayo yalikuwa yanatolewa na moja ya wakandarasi waliokuwa katika jengo hilo.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, akiendelea na ukaguzi.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, akikagua mazingira ya nje ya jengo hilo(juu na chini).
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, akiwaelekeza jambo wakandarasi wakati wa ukaguzi huo.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, akizungumza na Viongozi alioambatana nao katika ukaguzi huo.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt.
Mustapher Mohamed Siyani, akijadili jambo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu
Masjala Ndogo Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga pamoja na Msajili Mkuu wa Mahakama
Kuu ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya.
Habari hii imehririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni