Na MUKSINI NAKUVAMBA – Mahakama, Mbeya
Mahakama
ya Rufani ya Tanzania inayoketi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya imeanza
kuendesha Kikao chake cha kusikiliza mashauri 38 ya rufaa za madai na jinai
ambacho kimeanza jana tarehe 03 Agosti, 2026 na kinatarajiwa kuhitimishwa mnamo
tarehe 29 Agosti, 2026.
Kikao
hicho kinachoongozwa na Jopo moja la Majaji wa Mahakama ya Rufani ambalo Mwenyekiti
wake ni Jaji wa Rufaa ya Tanzania ya Tanzania, Mhe. Dkt. Gerald A. M. Ndika,
Majaji wengine katika Jopo hilo ni Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Dkt. Benhajj
Shaban Masoud na Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina.
Akiwasilisha
taarifa katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Mahakama Kuu Mbeya,
ambacho ni kikao cha maandalizi ya uendeshaji wa kikao hicho (Pre- Session
Meeting), Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Bernad
Mpepo alisema kuwa, jumla ya mashauri 38 ya rufaa za madai na jinai yamepangwa
kusikilizwa katika Masjala Ndogo ya Mbeya ikiwa rufaa za madai ni 27 na rufaa
za jinai 11.
Aidha,
Mhe. Mpepo aliongeza kuwa, Katika kikao hicho kinachoketi Mbeya pia kuna
mashauri kutoka Kanda za Songwe, Tabora na Iringa na katika kuhakikisha ufanisi
wa kikao hicho na kufikiwa kwa malengo yaliyokusudiwa ratiba ya kikao ilitolewa
kwa wakati na hati za kuitwa shaurini za wadaawa kwa ajili ya usikilizwaji wa
mashauri zimesambazwa na juhudi za kuwapata wadaawa amabao hawajapatikana
zinaendelea.
Naye,
Mwenyekiti wa kikao hicho, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Dkt. Gerald A. M.
Ndika, alisisitiza kuhusu kuzingatia upachikaji wa nyaraka zote muhimu
zinazohitajika hasa nyaraka zinazopandishwa kielektroniki kuhakikisha kuwa,
zinaambatanishwa pia kama nyaraka ngumu kwenye vitabu na majalada husika.
Aidha,
Mhe. Dkt. Ndika alihitimisha kwa kuomba ushirikiano baina ya wadau na
kusisitiza kufuata kanuni na sheria ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
“Ninawashukuru
sana kwa kuhudhuria kwenu, tufuate kanuni na tushirikiane ili tufikie mafanikio
yaliyokusudiwa. Lengo letu ni kutafuta haki kwa pamoja na ni matarajio yetu kuwa, kutokana na kwamba mpango wa kusikiliza mashauri haya uliandaliwa mapema pamoja kwa ufuatiliaji wa karibu wa kila jalada, kikao hiki kitafikia malengo
yaliyokusudiwa bila akukwama,” alisema Mhe. Dkt. Ndika.
Kwa upande
wao Jeshi la Magereza kupitia mwakilishi wa Mkuu wa Gereza Ruanda Mbeya alisema
kuwa, watahakikisha wafungwa wanafikishwa kwa wakati mahakamani na watahakikisha
wanatoa kibali kwa mawakili kuwaona wateja wao walipo gerezani hata kwa siku za
mapumziko ambazo ni jumamosi na jumapili ili kuweka utaratibu sawa.
Kikao
hicho kilihudhuriwa pia na Viongozi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya
akiwemo Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya,
Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Mussa Pomo, Jaji wa Mahakama
Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Angaza Mwipopo, Mtendaji wa Mahakama Kuu
Masjala Ndogo ya Mbeya Bw. Festo Chonya, Naibu Msajili Mahakama Kuu Masjala
Ndogo ya Mbeya Mhe. Bernad Mpepo, Naibu Msajili Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya
Mhe. Zawadi Laizer, Mawakili na Wadau wengine wa Haki Jinai na madai kutoka
Mbeya, Songwe na Tabora.
Mwenyekiti
wa jopo la Waheshimiwa Majaji wa
Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Dkt. Gerald A. M. Ndika, (katikati) akiongoza kikao cha wadau cha
uendeshaji wa shauri ya rufaa za Mahakama ya Rufani, kulia ni Jaji wa
Mahakama ya Rufani Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina na kushoto ni Jaji wa
Mahakama ya Rufani Mhe. Dkt. Benhajj Shaban Masoud
Naibu
Msajili Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Bernad Mpepo akiwasilisha
taarifa ya mashauri yanayotarajiwa kusikilizwa katika kikao hicho.
Sehemu
ya Viongozi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya wakiongozwa na (wa kwanza
kulia) ambaye ni Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Fahamu Mtulya, Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Angaza Mwipopo
(aliyesimama katikati) na Jaji wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe.
Mussa Pomo (wa kwanza kushoto).
Sehemu
ya wadau walioshiriki katika kikao hicho.
Sehemu
ya wadau walioshiriki katika kikao hicho
Sehemu
ya wadau walioshiriki katika kikao hicho
Jopo
la Majaji watatu wa Mahakama ya Rufani Tanzania wakipokelewa na Waheshimiwa
Majaji, Mahakimu na watumishi wengine wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya walipowasili katika viwanja vya Mahakama hiyo.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha- Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni