Ijumaa, 14 Agosti 2026

MASJALA NDOGO SONGWE YAANZISHA PROGRAMU YA MAZOEZI KUIMARISHA AFYA

Na IMAN MZUMBWE - Mahakama, Songwe

Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Songwe imeanzisha programu maalum ya mazoezi ya viungo ili kujenga utimamu wa mwili ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kujiandaa na mashindano mbalimbali, kuimarisha afya na kuongeza mshikamano miongoni mwa watumishi wa Mahakama. Programu hayo ya mazoezi itakuwa inafanyika katika viunga vya Mahakama Kuu iliyopo Nselewa-Mlowo.

Programu hiyo ya mazoezi inafanyika kwa kuwashirikisha watumishi mbalimbali wa Mahakama na wadau ambao wanapata nafasi ya kufanya mazoezi ya viungo na michezo mbalimbali chini ya usimamizi wa viongozi wa michezo ambao ni Afisa michezo Bi. Collether Amos Carlos, Mwenyikiti wa michezo Bw. Iman Patson na Katibu wa michezo Bi. Joyce Simba.

Akizungumza wakati wa kuanza mazoezi hayo, Afisa Michezo Bi. Collether Amos Carlos, amewaasa na kuwahimiza watumishi kujitokeza kwa wingi kushiriki kikamilifu katika mazoezi hayo na akisisitiza kuwa, michezo ni muhimu katika kuimarisha afya, kujenga umoja, ushirikiano na kuongeza morali ya utendaji kazi.

Aidha, Bi. Collether ameongeza kuwa, mazoezi hayo yataendelea kwa utaratibu maalum ili kuhakikisha watumishi wanakuwa katika hali nzuri kiafya na kuwa tayari kushiriki katika mashindano mbalimbali yatayokutanisha watumishi wa Mahakama na wadau wengine, huku Kaulimbiu ya programu hiyo ikiwa ni; “Afya bora, umoja na ushiriakiano kwa utendaji bora wa kazi”.

Afisa Michezo Bi. Collether Amos Carlos wa (kwanza kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama Songwe.

Mwalimu wa michezo Bw. Martin Pales Kambengwa akitoa mazoezi mbele ya watumishi wa Mahakama ambao hawapo katika picha.

Watumishi wa Mahakama wakifanya mazoezi ya kucheza mpira wa mikono yaani netball

Watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Songwe wakifanaya mazoezi mepesi (warm up)

Watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Songwe wakifanaya mazoezi mepesi ya kupasha misuli.


 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni